Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji Dk. Mary Nagu akimsikiliza aliyekuwa Mwakilishi Mkuu wa Uchumi na Biashara wa watu wa Jamhuri ya China nchini, Zhao Zhongqiu, alipokwenda ofisini kwake kumuaga .
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji Dk. Mary Nagu akisalimiana na Mwakilishi Mkuu mpya wa Uchumi na Biashara wa watu wa Jamhuri ya China nchini, Lin Zhiyong leo, ofisini kwake jijini Dar es Salaam, alipokwenda kujitambulisha kwake. Kulia ni Zhao Zhongqiu, aliyemaliza muda wake wa kufanya kazi hapa nchini.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji Dk. Mary Nagu, akizungumza na ujumbe wa wawakilishi wa Uchumi na Biashara wa watu wa Jamhuri ya China nchini Tanzania, kuhusu masuala mbalimbali, ikiwa ni pamoja na jinsi ya kuimarisha mahusiano ya kiuchumi na kibiashara kati ya Tanzania na China.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji Dk. Mary Nagu, akiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi hao, mara baada ya kuwa na mazungumzo nao.






No comments:
Post a Comment