Wanajeshi wakiwaondoa raia wa Sudan Kusini kutokana na mapigano
yanayoendelea
Wakati juhudi zikizidi kuendelea za kujaribu kumaliza mapigano
Sudan Kusini, Msemaji wa Jeshi la Sudan Kusini amesema kuna matumaini madogo ya
kusitishwa kwa mapigano.
Machar aliyasema hayo baada ya serikali kusema ipo tayari kusitisha mapigano makubaliano yaliyopokewa kwa mikono miwili na viongozi wa Afrika Mashariki mjini Nairobi.
Mapigano yaliendelea siku ya ijumaa katika mji wa Makalal, katika jimbo la Upper Nile.
Tayari askari zaidi wa Umoja wa Mataifa wa kuongeza nguvu wamekwishawasili nchini Sudan Kusini.
No comments:
Post a Comment