TANGAZO


Friday, May 4, 2018

Bango lililoandikwa kwa Kichina Nairobi lazua mdahalo

Tangazo lenyewe

Haki miliki ya pichaHISANI
Bango la matangazo ambalo lilikuwa limeandikwa kwa Kichina na kuweka katika barabara kuu ya Mombasa kwenda Nairobi limeharibiwa na watu wasiojulikana.
Bango hilo liliharibiwa baada ya Wakenya mtandaoni kulalamika kuhusu tangazo hilo lililokuwa limeandikwa kila kitu kwa Kichina.
Ni nambari za simu ambazo zilikuwa zimeandikwa kwa herufi za Kilatini ambazo ziliweza kusomeka.
Mabaki ya bango hilo baada ya kuharibiwa
Image captionMabaki ya bango hilo baada ya kuharibiwa
Wakenya mtandaoni walilalamika ni vipi bango hilo 'lisiloeleweka' na wenyeji liliidhinishwa kuwekwa kwenye barabara hiyo bila kutafsiriwa kwa Kiingereza au Kiswahili.
Baadhi waliwaomba maafisa wakuu serikali wawasaidie kutafsiri:
Mtangazaji huyu alisema matangazo yanafaa kuwa kwa Kiingereza na Kiswahili na kupendekeza liondolewe.
Baadhi hata hivyo walitetea bango hilo wakisema huenda aliyeliweka aliwalenga Wachina pekee.
Miongoni mwa waliolalamika ni Shirikisho la Watumizi wa Bidhaa na Huduma Kenya (Cofek).
Presentational grey line

Nani aliweka tangazo hilo?

Tangazo hilo liliwekwa na kampuni ya ujenzi ya Yunnan International.
Presentational grey line

Tangazo hilo lilisema nini?

Tafsiri iliyofanywa na Idhaa ya Kichina ya BBC inaonesha linasema:
Yunnan International
Kituo cha huduma zote za ujenzi
  • Uanakandarasi
  • Masuala ya wafanyakazi
  • Bidhaa za ujenzi
  • Utengenezaji wa bidhaa
  • Utengenezaji wa chuma
  • Huduma za usalama
  • Matangazo
  • Ukarabati na utunzaji
  • Mnara wa maji na uhifadhi wa maji
Nambari ya simu ya moja kwa moja: 0708 848 008
Kampuni ya kuaminika na ya kusifika
Yenye kufanya kazi kwa utaalamu na njia bora zaidi
Huduma ya kiwango na ubora wa juu
Presentational grey line
Baadhi ya Wakenya mtandaoni waliingiza utani:

No comments:

Post a Comment