TANGAZO


Sunday, August 20, 2017

Iraq yafanya mashambulizi ya ardhini kuuteka mji wa Tal Afar kutoka IS

Iraqi armoured vehicles are transported to the frontline outside Tal Afar (15 August 2017

Haki miliki ya pichaAFP
Image captionIraq yafanya mashambulizi ya ardhini kuuteka mji wa Tal Afar kutoka IS
Wanajeshi wa Iraq na makundi ya wapiganaji yanaounga serikali mkono wameanza mashambulizi ya ardhini katika mji wa Tal Afar, mojawepo wa ngome zilizosalia mikononi mwa kundi la kigaidi la Islamic state.
Mji huo umekuwa chini ya udhibiti wa Islamic state tangu mwaka 2014.
Akihutubia taifa kupitia runinga,waziri mkuu Haider al-Abadi, amesema wapiganaji wa Islamic state huko Tal Afar wanafaa kujisalimisha ama wauwawe.
Shia paramilitary fighters take a rest during a live ammunition training exercise in Najaf city, southern Iraq, 14 August 2017Haki miliki ya pichaEPA
Image captionWapiganaji wa kiShia
Takriban wapiganaji 2000 wa Islamic state wanaaminika kuwa wamesalia katika mji huo, ambao umezingirwa tangu mwezi Juni, na umekuwa ukishambuliwa kutoka angani na ndege za kivita za Marekani na Iraq.
Raia Wengi walitoroka mji huo, japo 40,000 walibaki.
Ndege za jeshi la Iraq zimeshambulia ngome za IS katika mji huo kwa siku kadha, kuandaa mashambulizi ya ardhini
Map showing control of Iraq and Syria (14 August 2017)
Image captionIraq yafanya mashambulizi ya ardhini kuuteka mji wa Tal Afar kutoka IS

No comments:

Post a Comment