TANGAZO


Tuesday, July 4, 2017

Korea Kaskazini yajivunia jaribio ya kombora la masafa marefu

Runinga ya Korea Kaskazini ikitangaza mafanikio ya majaribio ya ICBM
Korea Kusini inasema kuwa imefanikiwa kulifanya majaribio kombora la masafa marefu linalofahamika kama (ICBM)
Tangazo kwa njia ya runinga lilisema kuwa kombora hilo ambalo lilianguka katika bahari ya Japan siku ya Jumanne linaweza kushambulia popote pale duniani.
Lakini Marekani na Urusi zilisema kuwa kombora hilo lilikuwa la masafa ya wastani na halikuwa na tisho lolote kwa nchi zote mbili.
Korea Kaskazini imeongeza kasi ya kufyatua majaribio makombora yake na nuklia na kikiuka marufuku ya baraza la ulinzi la Umoja wa Mataifa.
North Korean TV releases photos of purported ICBM test launchHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionTelevisheni ya Korea Kaskazini ilitoa picha za majaribio ya ICBM
China na Urusi ziliitaka Korea Kaskazini kuachana na mipango yake ya nuklia.
Tangazo kwenye televisheni ya taifa nchini Korea Kaskazini ilisema kuwa majaribio ya kombora hilo la Hwasong-14 yalishuhudiwa na kiongozi Kim Jong-un.
Telivisheni ilisema kuwa kombora hilolilipaa umbali wa kilomita 2,802 na kusafiri umbali wa kilomita 933 kabla ya kuanguka baharini.

Kombora hilo lina uwezo wa kusafiri umbali gani?

Swali kuu ni kombora hili linaweweza kufika umbali gani? Lina uwezo wa kuanguka nchini Marekani?
David Wright ambaye ni mwafisikia kutoka Marekani, anasema kuwa ripoti hizo ni za ukweli, kombora hili linaweza kufika, umbali wa kilomita 6,700.
Uwezi huo utaliwezesha kufika Alaska lakini si majimbo mengine 48 ya Marekani.
Map showing estimates of North Korean missile ranges
Image captionRamani ya kuonyesha uwezo wa makombora ya Korea Kaskazini

Je majirani na nchi zenye nguvu za nyuklia zina wasiwasi?

Rais wa Korea Kusini Moon Jae-in, ametoa wito kwa baraza la ulinzi la Umoja wa Mataifa kuchukua hatua dhidi ya Korea Kusini.
Japan imesema kuwa uchokozi wa mara kwa mara kama huu ni kitendo kisichokubalika.
Map of Panghyon in North Korea
Image captionRamani ya Korea
Urusi na China wanasema kuwa majaribio haya hayakubaliki.
Rais wa China Xi Jinping yuko Moscow ambapo alifanya mazungumzo na Rais wa Urusi Vladimir Putin.
Viongozi hao wawili wameitaka Korea Kaskazini kuachana na majaribio yake.
North Korean TV releases photos of purported ICBM test launchHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMajaribio hayo yalishuhudiwa na Kim Jong-un
Rais wa Marekani Donald Trump mara kwa mara ameitaka china ambaye ni mshirika wa karibu na Korea, kuishinikiza kuachana na mpango wake wa nuklia.
Katika suala la Korea Kaskaznia kuwa na uwezo wa kushambulia Marekani, mwezi Januari Trump alindika, "hilo halitafanyika". Lakani hata hivyo wataalamu wanasema kuwa hilo huenda likawezekana, ndani ya miaka mitano au chini.
ICBM flight track
Image captionNjia ya ICBM
Key parts of an ICBM
Image captionSehemu za ICBM

No comments:

Post a Comment