TANGAZO


Saturday, October 8, 2016

Trump aomba radhi kwa kuwatusi wanawake

Donald Trump


Image copyrightAP

Mgombea urais wa chama cha Republican Marekani, Donald Trump, ameomba msamaha kwa matamshi machafu aliyotoa kuhusu wanawake katika kanda ya video iliyozuka ya miaka 11 iliopita.
Katika kanda hiyo, Trump anasikika akijigamba kuhusu kuwagusa wanawake sehemu zao za siri na kujaribu kushiriki ngono nao, anasema: 'unaweza kufanya chochote unapokuwa nyota'.
Maafisa wakuu wa chama cha Republican wameshutumu vikali matamshi yake akiwemo spika wa bunge, Paul Ryan, aliyesema amechafuzwa roho na matamshi hayo.
Mhariri wa BBC wa eneo la Amerika kaskazini anasema hiki ni kiwango cha mzozo katika azma ya Trump kuwania urais wa Marekani
Katika kanda iliyorekodiwa Trump aliomba radhi kwa kuonekana akisoma, na ameahidi kuwa mwanamume bora zaidi lakini amemshutumu Bill Clinton kwa kuwanyanyasa wanawake kingono.
Amemshutumu Hillary Clinton pia kwa kuwakandamiza na kuwaibisha waathiriwa wa unyanyasaji uliotekelezwa na mumewe.

No comments:

Post a Comment