TANGAZO


Wednesday, September 28, 2016

SSRA YAWAPIGA MSASA WAANDISHI WA HABARI KUHUSU HIFADHI YA JAMII, YAWATOA HOFU WANANCHI KUHUSU MIFUKO YA HIFADHI YA JAMII NCHINI

Mwanahabari Tuma Dandi, akitoa maelezo mafupi wakati akitoa salamu kutoka kwa waandishi kabla ya ufunguzi wa semina ya Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA) kwa waandishi wa habari kuhusu Hifadhi ya Jamii jijini Dar es Salaam leo.(Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhamasishaji wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Sarah Kibonde Msika, akizungumza wakati akiifungua semina hiyo. Kulia ni Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Mamlaka hiyo, Onorius Njole. 
Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Onorius Njole kitoa mada kuhusu miongozo inayopaswa kufuatwa na mifuko ya Hifadhi ya Jamii wakati wa semina hiyo ya siku moja ya wanahabari kuhusu mifuko ya jamii Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Uhamasishaji wa SSRA, Sarah Kibonde.
Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Onorius Njole kiwasilisha mada hiyo.
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mada hiyo, wakati wa semina hiyo.
Waandishi wa habari wakiwa katika semina hiyo, wakifuatilia mada hiyo.
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia mada hiyo, wakati wa semina hiyo.
Waandishi wa habari wakifuatilia kwa makini mada hiyo, wakati wa semina hiyo.
Waandishi wa habari wakinukuu baadhi ya maelezo yaliyokuwa yakitolewa katika mada hiyo.
Waandishi wa habari wakiwa katika semina hiyo.
Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Onorius Njole, akifafanua jambo wakati akiwasilisha mada.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhamasishaji wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Sarah Kibonde Msika, akizungumza na waandishi wa habari, alipokuwa akitoa ufafanuzi mara baada ya kuifungua semina hiyo jijini leo.
Mkurugenzi wa Tafiti, Sera na Tathmini wa SSRA, Ansgar Mushi akitoa mada katika semina hiyo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhamasishaji wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Sarah Kibonde, akiteta jambo na Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Onorius Njole (kushoto), wakati wa semina hiyo.
Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya jamii (SSRA)Sabato Kasuri (kulia), akiwa katika semina hiyo.
Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya jamii (SSRA)Sabato Kasuri akisimamia uulizwaji wa maswali kutoka kwa waandishi wa habari kuelekea kwa viongozi wa SSRA katika semina hiyo.
Mwandishi wa gazeti la Mwananchi Saumu Waziri akiuliza maswali wakati wa semina hiyo.
Baadhi ya viongozi wa SSRA, wakinukuu maswali ya waandishi wa habari.
Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Onorius Njole (kushoto), akijibu baadhi ya maswali ya waandishi wa habari.
Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya jamii (SSRA)Sabato Kasuri (kulia), akiwa katika semina hiyo.
Mkurugenzi wa Tafiti, Sera na Tathmini wa SSRA, Ansgar Mushi akijibu maswali ya waandishi wahabari, wakati wa semina hiyo.
Baadhi ya viongozi wa SSRA, wakiwa katika picha ya pamoja na waandishi wa habari, waliohudhuria semina hiyo, mara baada ya kufungwa rasmi.

Na Dotto Mwaibale
MAMLAKA ya Usimamizi wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii nchini (SSRA), imewataka Watanzania kuondoa hofu iliyojengeka kwenye jamii kuwa mifuko ya hifadhi ya jamii ina hali mbaya kifedha.

Akizungumza katika warsha maalum ya siku moja ya waandishi wa habari, iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa SSRA, Ansgar Mushi alisema kuwa mifuko hiyo haina hali mbaya kama wanavyodhani watu katika jamii kwani ina fedha za kutosha.

“Watanzania wamekuwa wakiambizana kuwa mifuko hii ina hali mbaya kifedha, napenda kuwahakikishia kuwa ina fedha za kutosha kwani tumekuwa tukifanya ukaguzi wa mara kwa mara. Katika kaguzi zetu za mara kwa mara hakuna mfuko tuliobaini kuwa una kasoro au upungufu wowote,” alisema Mushi.

Aidha, Mushi alisema kwa mwaka mifuko hiyo ya pensheni imekuwa ikikusanya jumla ya sh trilioni 1.692 wakati mfuko wa bima ya afya (NHIF) unakusanya sh bilioni 88.5 ambapo jumla ya makusanyo yote ni sh trilioni 1.78.

Kwa upande wa fao la kujitoa, Mushi alisema licha ya kutawaliwa na sintofahamu, fao hilo lilifutwa na Serikali kuanzia mwaka 2012 na kwa sasa SSRA imeanzisha mchakato wa kuratibu uanzishwaji wa fao la upotevu wa ajira.

Mushi alisema kuwa fao hilo lilipofutwa, bado kulikuwa na mifuko iliyoendelea kuruhusu kujitoa lakini kwa sasa wameamua waanzishe mchakato wa fao la kupoteza ajira, ambalo ni mahususi kwa ajili ya kuwanufaisha waathirika.

“Fao la Upotevu wa ajira litakuwa mahsusi kwa ajili ya wale waliopoteza ajira zao, huku wakiwa wamechangia mifuko ya hifadhi kwa kipindi cha miezi zaidi ya 18. Hawa watalipwa asilimia 33 ya mshahara wa mwisho kwa kipindi cha miezi 6,”

“Kipindi hicho cha miezi 6 kikiisha, mtu huyo kama hajapata ajira atawekwa katika hatua nyingine ambapo ataruhusiwa kuchukua nusu ya fedha alizochangia katika kipindi chake cha ajira,” alisema Mushi.

Akizungumzia wale waliopoteza ajira zao wakiwa hawajafikisha kipindi cha miezi 18, Mushi alisema kuwa wataruhusiwa kuchukua asilimia 100 ya fedha walizochangia kipindi chote walipokuwa kwenye ajira.

“Watu hao wataruhusiwa kuchukua fedha zao kwa asilimia 100 ambazo walichangia kipindi wakiwa waajiriwa. Hata hivyo, napenda kuwaambia Watanzania kuendelea kuichangia mifuko hiyo kwani ina manufaa zaidi nyakati za uzeeni baada ya kustaafu,” alisema Mushi.(Habari na Dotto Mwaibale)

No comments:

Post a Comment