Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Taasisi ya Kifedha ya UTT-Microfinance, Bw. James Washima akifuatilia hotuba ya Mgeni rasmi(hayupo Pichani) wakati mgeni huyo akifunga mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana wahitimu wa elimu ya juu nchini. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Rais wa Kujitegemea Bi.Haigath Kitala.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana kutoka Ofisi ya waziri mkuu Sera,Uratibu,Bunge,kazi,Ajira na Vijana Bw.James Kajugusi akizungumza katika kilele cha mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana wahitimu wa elimu ya juu nchini yaliyofanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam.
Kikundi cha wahitimu wa elimu ya juu SUJA ECO-ENERGY wakiwa na mfano wa hundi ya dola 3000 ambayo wamekabidhiwa baada ya kubuni wazo la kijasiriamali la mradi wa kutengeneza nishati kupitia kinyesi cha ng’ombe.
Kikundi cha wahitimu wa elimu ya juu cha RECHA wakikabidhiwa mfano wa hundi ya dola 3000 kutoka kwa Mkurugenzi wa Teknolojia na Operesheni wa Benki ya Posta Tanzania Bw.Jema Msuya. Benki ya Posta Tanzania ni moja ya waliodhamini mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana wahitimu wa elimu ya juu.
Kikundi cha wahitimu wa elimu ya juu cha GBL
Bucket Toilet Co. wakiwa katika picha ya pamoja na mwakilishi kutoka mfuko wa
ubunifu wa maendeleo kwa binadamu (HDIF)Bw. David McGinty baada ya kujishindia
dola 3000.Wahitimu hao wameshinda pesa izo baada ya kubuni mradi wa kutengeneza
choo ambacho kinatumia ndoo ya plastic.
Na Daudi Manongi-Maelezo, Dar es Salaam
19.09.2016
SERIKALI kupitia Baraza
la Taifa la Uwezeshaji wananchi kiuchumi limesema kuwa litaendelea kushirikiana
na wadau mbalimbali wa maendeleo nchini ili kutatua changamoto ya ajira kwa vijana.
Hayo yamesemwa juzi
Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Vijana katika Ofisi ya Waziri Mkuu, James Kajugusi wakati alipokuwa akifunga mafunzo ya ujasiriamali kwa
vijana wahitimu wa elimu ya juu nchini.
“Uwezeshaji wananchi kiuchumi
ni dhana pana inayohitaji ushirikiano wa karibu kati ya serikali na sekta binafsi
pamoja na wadau wa maendeleo na katika kuchochea juhudi za uwezeshaji wananchi kiuchumi”
alisemaBw.Kajugusi.
Akizungumzia kuhusu changamoto
zinazowakabili vijana nchini, Kajugusi alisema kuwa changamoto ya ukosefu wa ajira
kwa vijana imechochewa na mabadiliko ya kisera na kiuchumi yanayosimamiwa kwa dhati
na serikali katika kupeleka mbele zaidi taifa letu katika nyanja za kijamii na
kiuchumi.
Awali akizungumza na vijana
22 waliohitimu mafunzo hayo aliwataka vijana hao kuongeza ari ya kufanya kazi
na kushiriki fursa mbalimbali zinazojitokeza
zenye lengo la kujikwamua kiuchumi.
“Vijana mtumie vema fursa
mbalimbali za uwezeshaji mnazozipata kwa kuboresha zaidi uelewa wenu na hali zenu za maisha” Alisema
Kajugusi.
Kwa upande wake Kaimu
Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji wananchi kiuchumi, Bi Anna Mtaita amesema kuwa Baraza hilo
litaendelea kuthamini nchini na kwa
kulitambua hilo maana wameamua kushirikiana na taasisi ya maendeleo ya
Cambridge katika kuratibu na kutoa mafunzo hayo.
Mtaita aliongeza kuwa
mbali na programu hiyo, Baraza hilo pia linaratibu programu ya majaribio kwa vijana
walio katika mazingira magumu katika kuwapatia mafunzo, malezi, na kuwaunganisha
na mitaji.
Kwa mujibu wa Mtaita
alisema mpaka kufikia sasa Baraza hilo limewawezesha vijana 500 nchini katika
upataji wa mafunzo, malezi na mitaji.







No comments:
Post a Comment