Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga akimueleza jambo Afisa Mfawidhi wa Kambi ya kulea wazee ya Sukamahela Bw. Jeremiah Paul
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga akiongea na Wazee wanaoishi katika kambi ya kulea wazee ya Sukamahela na kuwaeleza dhumuni la serikali la kuzisaidia kambi hizo.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga akimkabidhi moja ya Mzee katika kambi ya wazee ya Sukamahela boksi la sabuni kwa niaba ya wazee katika kituo hicho chenye jumla ya wazee 67. Viongozi wa Kambi ya kulea Wazee ya Sokamahela wakimuonesha Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga baadhi ya nyumba wazazoishi wazee ambapo sehemu ya nyumba hizo zipo kwenye hali mbaya za kuhitaji marekebisho.
Viongozi wa Kambi ya kulea Wazee ya Sokamahela wakimuonesha Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga baadhi ya nyumba wazazoishi wazee ambapo sehemu ya nyumba hizo zipo kwenye hali mbaya za kuhitaji marekebisho.
Viongozi wa Kambi ya kulea Wazee ya Sokamahela wakimuonesha Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga baadhi ya nyumba wazazoishi wazee ambapo sehemu ya nyumba hizo zipo kwenye hali mbaya za kuhitaji marekebisho.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga akisalimiana na Bi. Theresia Msiwa anayeishi katika kambi ya kulea wazee ya SukaMahela iliyopo Wilayani Manyoni Mkoani Singida.
Baadhi ya Wazee wanaoishi katika kambi ya Sukamahela iliyopo Wilayani Manyoni Mkoani Singida.
Jengo la Zahanati ya Serikali ya Sukamahela iliyo karibu na kituo hicho ambayo pia inasaidia kutoa kuhuma za matibabu kwa wazee wa kituo hicho.
Muuguzi katika Zahanati ya Sukamahela Bi.Marry Sailale akimpa maelezo Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga wa shughuli mbalimbali anazofanya ikiwemo kuwahudumia Wazee wanaoishi katika kambi ya Wazee ya Sukamahela iliyopo Wilayani Manyoni Mkoani Singida.
Muuguzi katika Zahanati ya Sukamahela Bi.Marry Sailale akisalimiana na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga alipotembelea kambi ya kulea wazee ya Sukamahela iliyopo Wilayani Manyoni Mkoani Singida.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga akiwaaga Wazee katika kambi ya kulea wazee ya SukaMahela baada ya kutembelea na kuona hali halisi ya Mazingira katika kambi hiyo.
Baadhi ya nyumba zilizo katika kambi ya kulea wazee ya sukamahela iliyopo Wilayani Manyoni Mkoani Singida. Baadhi ya nyumba zilizo katika kambi ya kulea wazee ya sukamahela iliyopo Wilayani Manyoni Mkoani Singida.
Baadhi ya nyumba zilizo katika kambi ya kulea wazee ya sukamahela iliyopo Wilayani Manyoni Mkoani Singida.
Katibu
Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba
Nkinga akimpa maelekezo Afisa Mfawidhi wa kambi ya kulea wazee ya Sukamahela iliyopo
Wilayani Manyoni Mkoani Singida Bw. Jeremiah Paul (kushoto)na kumtaka kuwa
makini katika kupokea Wazee katika kambi hiyo kwani kumekuwa na tabia ya Vijana
wenye uwezo kupeleka wazazi wao kwenye kambi hizi na kukwepa jukumu la kuwalea,Kulia
ni Bw. Richard Mallya Mkurugenzi Idara ya Ununuzi na Ugavi kutoka Wizara hiyo. (Picha zote na Hassan Silayo-MAELEZO)
Na
Hassan Silayo-MAELEZO
KATIBU Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba
Nkinga amewataka watanzania hasa vijana wenye uwezo, wanaopekea na kukaa na wazee
wao kwenye kambi za kulea wazee kuacha mara moja tabia hiyo.
Akiongea
wakati alipotembelea kambi ya kulea ya wazee ya Sukamahela iliyopo Wilayani
Manyoni Mkoani Singida Bi. Sihaba alisema kuwa Serikali
itaanza kuwachukulia hatua za kisheria watanzania wenye tabia hiyo kwani
kufanya hivyo ni kukiuka sheria ya wenye ulemavu na wazee inayowataka
wanafamilia kuwa na jukumu la kwanza la kumlea mzee na mtu mwenye ulemavu.
“Kumekuwa
na utamaduni kwa baadhi ya vijana nchini kupeleka wazee kwenye hizi kambi za
kulea wazee huku vijana hao wakionekana na kuwa na uwezo wa kuwalea, kwa kweli
huu utaratibu sisi kama serikali hatuwezi kuuvumilia kwanza ni ukiukwaji wa
sheria ya watu wenye ulemavu na wazee inayowataka wana familia kuwa na jukumu
la kuwalea wazee, hivyo ni matarajio yetu kuwa kijana amlee mzee wake kama
alivyolelewa yeye, Sisi kama serikali tutachukuwa jukumu la kuwalea wazee na
watu wenye ulemavu wanaotoka kwenye familia zisizo na uwezo kabisa”. Alisema
Bi. Sihaba.
Bi.
Sihaba aliongeza kuwa utamaduni huo pia unawanyima fursa Wazee na watu wenye
ulemavu wanaotoka kwenye familia zisizo na uwezo kupata huduma kutokana na
baadhi ya watu kukwepa majukumu yao ya kifamilia wakati wanauwezo wa kufanya
hivyo na kuzifanya kambi hizo kujaa na kushindwa kupokea watu wenye uhitaji.
Aidha,
Bi. Sihaba alisema kuwa Serikali ya awamu ya tano itaendelea kusimamia azma
yake ya kuisaidia wazee na watu wenye ulemavu nchini ili kuhakikisha inapunguza
na kuondoa kabisa changamoto zinazokabili kundi hilo.
Naye
Afisa Mfawidhi wa Kambi hiyo Bw. Jeremiah Paul ameishukuru serikali kwa kuona
umuhimu wa kuzisimamia ipasavyo kambi hizi kwani itasaidia kuondoa kabisa
changamoto zinazowakabili Wazee na watu wenye ulemavu katika maeneo hayo.
Akizungumza
kuhusuutoaji huduma za Afya kwa Wazee wa Kambi hiyo Muuguzi wa Zahanati ya
Serikali ya Sukamahela iliyokaribu na Kambi hiyo Bi Marry Sailale ameishukuru
serikali kwa kuona umuhimu wa kujenga zahanati hiyo karibu na kambi ya Wazee na
kuomba kuongezewa vifaa na wafanyakazi katika zahanati hiyo ili kuongezea
ufanisi katika kuwahudumia wazee wanaohitaji uangalizi wa karibu.
No comments:
Post a Comment