Bw. Ibrahim Mkwawa, Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa Upande wa Uperembe “Monitoring” (katikati) akikagua nyaraka mbalimbali za Chama cha Sauti ya Umma (SAU) wakati wa uhakiki wa utekelezaji wa masharti ya usajili na matakwa ya Sheria ya Vyama vya Siasa lililoanza leo, Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mhasibu, Bi. Severa Assey kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa.
Bw.Willy Brown Nyantiga, Mhasibu kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini akihoji taarifa za fedha wakati wa zoezi la kuhakiki utekelezaji wa masharti ya usajili na matakwa ya Sheria ya Vyama vya Siasa kwa Chama cha NLD Jijini Dar es Salaam leo. Katikati ni Mwenyekiti wa chama hicho, Bw. Oscar Emmanuel Makaidi na Katibu Mkuu wa chama hicho na kulia ni Bw. Tozzy Ephraim Matwanga.
Baadhi ya viongozi wa Chama cha Sauti ya Umma (SAU), wakifuatilia maelekezo kutoka kwa Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa Upande wa Uperembe, Bw. Ibrahim Mkwawa (hayupo pichani), wakati wa uhakiki wa utekelezaji masharti ya usajili na matakwa ya Sheria ya Vyama vya Siasa lililoanza leo, jinini Dar es Salaam.
Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa Upande wa Uhakiki wa Vyama vya Siasa, Bw. Sisty Nyahoza (wa tatu kulia), akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Chama cha National League for Democratic (NLD), wakati wazoezi la kuhakiki utekelezaji wa masharti ya usajili na matakwa ya Sheria ya Vyama vya Siasa Jijini Dar es Salaam leo.
Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa Upande wa uperembe, Ibrahim
Mkwawa (wa kwanza kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Chama
cha Sauti ya Umma (SAU), wakati wa zoezi la kuhakiki utekelezaji wa masharti ya usajili na matakwa ya Sheria ya Vyama vya Siasa Jijini
Dar es Salaam leo.(Picha zote na Maelezo)
No comments:
Post a Comment