TANGAZO


Sunday, June 26, 2016

RAIS DK. MAGUFULI AZINDUA MPANGO WA USALAMA WA JAMII UNAOSIMAMIWA NA JESHI LA POLISI



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na hafla ya wakazi wa jiji la Dar es salaam wakati wa uzinduzi wa Mpango wa Usalama wa Jamii unaosimamiwa na Jeshi la Polisi nchini leo jijini Dar es Salaam.(Picha zote na Eleuteri Mangi)

Baadhi ya wageni waalikwa wakimsikiliza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakati wa uzinduzi wa Mpango wa Usalama wa Jamii unaosimamiwa na Jeshi la Polisi nchini leo jijini 
Dar es salaam.

Baadhi ya askari wakitoa heshima wakati wimbo wa taifa unaimbwa kabla ya uzinduzi wa Mpango wa Usalama wa Jamii unaosimamiwa na Jeshi la Polisi nchini leo jijini
 Dar es salaam.

Kikundi cha Jeshi la Polisi wakitumbuiza kwa ngoma ya “makirikiri” uzinduzi wa Mpango wa Usalama wa Jamii unaosimamiwa na Jeshi la Polisi nchini leo jijini 
Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba (kushoto) wakati wa uzinduzi wa Mpango wa Usalama wa Jamii unaosimamiwa na Jeshi la Polisi nchini leo jijini Dar es salaam. Kulia ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini 
Inspekta Jenerali (IGP) Ernest Mangu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa Mpango wa Usalama wa Jamii unaosimamiwa na Jeshi la Polisi nchini. Wa kwanza kushoto mwa Rais ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mwigulu Nchemba na wa kwanza kulia mwa Rais ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Inspekta Jenerali (IGP) Ernest Mangu. 


Moja ya vituo vya Polisi vinavyohamishika ambacho Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amekizindua jijini Dar es Salaam.


Na Jonas Kamaleki

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli amelitaka jeshi la polisi nchini kuwadhibiti majambazi ipasavyo kwa kuwanyanganya silaha kwenye matukio ya kiuharifu ili kukomesha vitendo viovu katika Taifa.


Rais Magufuli ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Mpango wa Usalama wa Jamii.


“Inashangaza jambazi anavamia kituo cha polisi anaua na anaondoka wakati polisi wapo na wana silaha na risasi wanazo lakini wanashindwa kumnyang’anya silaha,”alishangaa Rais Magufuli.


Ameongeza kuwa ujambazi na vitendo vya uharifu nchini inabidi vikomeshwe mara moja ili watanzania waishi kwa amani na kufanya maendeleo kwani wananchi wanataka maendeleo.


Akiongelea kuhusu maslahi na vitendea kazi kwa jeshi la polisi, Rais Magufuli amesema kuwa serikali yake itafanya kila iwezalo kuliwezesha jeshi hilo ili liweze kufanya kazi kwa ubora zaidi.


Rais Magufuli ameonyesha kuwa na imani na jeshi la polisi licha ya kuwa na kasoro ndogo ndogo kwa baadhi ya polisi ambao wanalichafua jeshi hilo.


Aidha ametoa agizo kwa TCRA kushirikiana na jeshi la polisi nchini ili kuweza kurekodi simu na kutoa print out mara moja tofauti na ilivyo sasa.

Kuhusu kundi la wafanyakazi wanaofanyakazi kwenye Dawati la Taarifa la polisi, Mhe. Rais amemtaka Mkuu wa Jeshi hilo, IGP Ernest Mangu kuwafikiria na kuwapatia posho ya kazi kwani kazi wanayoifanya ni ngumu mno na inahitaji umakini zaidi.


Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amemwomba Mhe. Rais kuliongezea fedha jeshi hilo ili liweze kufanya kazi kwa ustadi zaidi na kukomesha vitendo vya uharifu nchini.


Makonda amelipongeza jeshi la polisi kwa kudhibiti matukio ya ujambazi hapa nchini hususan kwenye mabenki.


Mpango huu wa Usalama wa Jamii umezinduliwa leo na utadumu hadi 2019 na unatarajiwa kutoa matokeo makubwa ya kudhibiti uharifu nchini.

No comments:

Post a Comment