TANGAZO


Monday, June 27, 2016

OFISI YA TAIFA YA TAKWIMU KUKUTANA NA WADAU PAMOJA NA WANANCHI JUMANNE JUNI 28, 2016 KWA AJILI YA KUTOA ELIMU NA KUSIKILIZA HOJA NA MAONI KUHUSU UTOAJI WA TAKWIMU RASMI NCHINI

Taarifa kwa Umma

Katika kuazimisha “WIKI YA UTUMISHI WA UMMA” yenye kauli mbiu “Uongozi wa Umma kwa ukuaji Jumuishi: kuelekea katika Afrika tunayoitaka”, Ofisi ya Taifa ya Takwimu inawajulisha wananchi na wadau wote kuwa imetenga siku ya Jumanne tarehe 28 Juni, mwaka huu, kuwa siku maalumu ya kukutana na wananchi ili kutoa elimu na kusikiliza hoja na maoni kuhusu utoaji wa takwimu rasmi nchini.

Muda ni kuanzia saa 3.00 Asubuhi hadi saa 9.00 Alasiri katika ukumbi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Makao Makuu.

KARIBUNI WOTE
ImetolewanaMkurugenzi Mkuu,
OfisiyaTaifayaTakwimu.

24June, 2016     

No comments:

Post a Comment