Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Bi.Joselin Lugola akitoa mrejesho kuhusu nyumba za shirika hilo zilizo kisarawe mkoani Pwani ikiwemo kukamilisha upatikanaji wa hati wa eneo hilo na kuliendeleza ili watumishi wa TBC wa kisarawe walitumie kwa makazi.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Anastazia Wambura (wa pili kushoto) akipata msaada wakati akiteremka toka katika kiwanja cha Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kulipojengwa nyumba za watumishi wa shirika hilo, ambazo hazijaisha kwa zaidi ya miaka 20 sasa na kutoa maagizo ya kumalizia nyumba hizo au kuwapa Halmashauri ya Kisarawe ili wajenge Hostel za wanafunzi.
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe Anastazia Wambura akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Bi.Joselin Lugola wakati alipofanya ziara katika nyumba za shirika hilo zilizopo kisarawe mkoani Pwani.
Na Daudi Manongi-WHUSM
NAIBU Waziri Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na
Michezo Mhe.Anastazia Wambura ametoa wito kwa Shirika la Utangazaji Tanzania(TBC)
kutunza Rasilimali za Taifa kwa kuwa ni pesa inayotoka na jasho la mlipa Kodi
na ingeweza kutumika kwa kazi nyingine kuliko uharibifu unaofanyika katika
kiwanja cha shirika hilo kilicho eneo la Kimani ambako zimejengwa nyumba za
wafanyakazi wa shirika hilo, waliopo kisarawe Mkoa wa Pwani.
Mhe.Wambura
alisema hayo wakati alipotembelea eneo la shirika hilo ili kupata mrejesho wa
maagizo aliyotoa wakati alipofanya ziara ya kwanza katika eneo hilo Aprili 2011
mwaka huu na kuipatia siku saba Idara ya Miradi ya shirika hilo ikishirikiana
na Halmashauri ya Kisarawe kufanikisha upatikanaji wa hati miliki ya eneo hilo
la makazi ya wafanyakazi wa shirika hilo.
“Taratibu
za Kisarawe za upatikanaji wa hati zimekamilika na sasa wamepeleka ile Rasimu
kwa kamishna wa hati Kanda ya Mashariki na maelezo tumeyaskia kwamba kulikuwa
na kupishana katika uaandaaji wa hati ndo maana ikachelewa lakini kwa sasa hivi
bado tunaitaji kulinda rasilimali za Taifa.Tunaitaji kuzuia uhalibifu”. Alisema
Mhe Wambura.
Aidha
Mhe Wambura ametoa maagizo kwa shirika hilo kuangalia uwezekano wa kuendeleza
makazi hayo kwa kuwa mpaka sasa imepita miaka 20 eneo hilo halijaendelezwa na
shirika hilo au kufanyiwa uwekezaji wowote au wakabidhi eneo hilo kwa
halmashauri ya Kisarawe ili wajenge hostel za wanafunzi na kuongeza kwamba yeye
hatakubali eneo hilo lipotee kwa uharibifu kwa wananchi kubomoa nondo na kuuza kama vyuma chakavu.
Kwa
upande wake Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu wa Shirika la Utangazaji
Tanzania(TBC) Bi.Joselin Lugola alimwahidi waziri huyo kuwa watahakikisha
kwenye bajeti ya mwaka 2017/18 suala hilo linashughulikiwa na kudai kwamba mara nyingi wanaweka pesa ya
ukarabati lakini inakatwa lakini wataanza ukarabati kwa awamu kwa mikoa ya
Arusha na Mwanza na makao makuu kwa hiyo hata izi za kisarawe zitakarabatiwa
mara moja.
No comments:
Post a Comment