Katibu Mkuu wa Uchukuzi Dkt Leonard Chamriho (kulia), akipatiwa maelezo.
Katibu Mkuu wa Uchukuzi Dkt Leonard Chamliho akipanda ngazi kuelekea kwenye pambu na valvu zilizofungwa kwenye mita ya kupimia mafuta(Flow Meter) wakati alipofanya ziara ya kushtukiza kukagua utendaji kazi wa mita hiyo leo Mei 18,2016.
Meneja Mradi /msimamizi wa Ujenzi wa mradi wa Mita za kupimia mafuta Mhandisi Mary Mhayaya (kushoto) akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa Uchukuzi Dkt Leonard Chamliho (wa pili kushoto) kuhusu hitilafu iliyojitokeza katika moja ya valvu zilizoko kwenye mita hiyo, upande unaoendeshwa kwa kutumia mfumo wa digitali hali iliyosababishwa na mvua zilizokuwa zikiendelea kunyesha hivi karibuni Jijini Dar es Salaam.Mita hiyo sasa inatumia mfumo wa analojia na hatua ya urejeshaji wa valvu hiyo katika hali yake ya awali inafanyiwa kazi na mkandarasi aliyepewa zabuni ya kujenga mita hiyo leo.
Katibu Mkuu wa Uchukuzi Dkt Leonard Chamliho ( wa pili kulia) akitoa maagizo kwa Mamlaka ya Bandari kuyafanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza ikiwemo hitilafu ya kamera za ulinzi na baadhi ya valvu kwenye mita ya kupimia mafuta na kuwasilisha taarifa ofisi kwake Jumatatu Mei 23 namna ya watakavyoshughulikia mapungufu yaliyojitokeza.
Mita ya Kupimia Mafuta (Flow Meter) iliyojengwa eneo la kwa mwingira, mji Mwema Kigamboni Jijini Dar es salaam . Utaratibu wa kujenga uzio na paa kufunika mtambo huo unaendelea kupitia mkandarasi aliyepewa jukumu la kujenga mradi huo ili kuhimarisha ulinzi na usalama wa mita hiyo.(Picha zote na Raymond Mushumbusi na Aron Msigwa-Maelezo)
Na Lorietha Laurence - Maelezo,Dar es Salaam.
KATIBU Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi
na Mawasiliano (Uchukuzi) Mhandisi Dkt. Leornad Chamuriho ameupa siku mbili
uongozi wa Bandari unaosimamia Mita ya Kupimia mafuta nchini (Flow Meter)
iliyoko Kigamboni jijini Dar es Salaam kuhakikisha kuwa unatoa taarifa ndani ya
siku mbili kuhusu hitilafu iliyojitokeza kwenye mfumo wa kufungua valvu za mita
hiyo upande wa umeme.
Aidha, ameuagiza uongozi huo kutoa taarifa
kuhusu hitilafu ya kamera 2 za usalama zilizoungua na kushindwa kufanya kazi
kwa takribani mwezi mzima.
Katibu
Mkuu huyo ametoa maagizo hayo mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika
mita hiyo eneo la mji Mwema Kigamboni leo jijini Dar es salaam na kubaini
upungufu wa utendaji wa baadhi ya maeneo.
Maeneo
hayo ni pamoja na kamera za kufuatilia mwenendo wa usalama wa mita hiyo,
valvu zilizoshindwa kufanya kazi upande wa mfumo wa umeme hivyo kubakiwa
na njia ya analoji kutokana na hali ya mvua zilizokuwa zikiendelea kunyesha
jijini Dar es salaam.
“Ifikapo Jumatatu nipatiwe taarifa kuhusu matengenezo ya vifaa hivi, hatua
zilizochukuliwa na mnieleze lini ukarabati wake utakamilika pia ujenzi wa paa
kuzuia athari ya mvua kwenye mita hii” amesema Dkt. Chamuriho.
Ameongeza
kuwa dhumuni la Serikali ni kuhakikisha vifaa hivyo vinafanya kazi katika
viwango vinavyostahili ili kulinda mapato yanayotokana na mafuta yanayoingia
nchini ili Serikali ipate kodi halali na hivyo kuongeza mapato ya nchi na
kuondoa malalamiko kwa wateja.
Kwa
upande wake Meneja Mradi wa Ujenzi wa Mita hiyo kutoka Mamlaka ya
Bandari nchini Mhandisi Mary Mhayaya ameeleza kuwa uharibifu wa vifaa hivyo
umesababishwa na mvua zilizonyesha hivi karibuni na tayari vifaa hivyo
vimeanza kukabarati.
"Kisichofanya kazi ni mfumo wa kufungua mafuta upande wa umeme kwenye baadhi ya
valve, upande wa analoji unafanya kazi vizuri na kazi ya upakuaji mafuta
kupitia mfumo wa analojia inaendelea kama kawaida" Amesisitiza.
Amesema
kuwa tayari wamemweleza mkandarasi aliyefunga vifaa hivyo kuvifanyia
marekebisho haraka iwezekanavyo.
Naye
Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) Hebel Mhanga amesema kuwa
ofisi yake inajukumu la kuhakikisha inatoa huduma sahihi kwa wateja wanaotumia
mitambo hiyo iliyopo bandarini hapo na Serikali inapata mapato kulingana
na huduma iliyotolewa.
Mita
ya Kupimia Mafuta yalnayoingia nchini iko katika hatua ya majaribio kwa kipindi
cha mwaka mmoja ambapo tayari meli tatu zimefanyiwa majaribio ya upakuaji wa
mafuta huku moja ikiwa imefanyiwa vipimo.

No comments:
Post a Comment