
Dereva wa teksi ya kampuni ya Uber jana usiku aliteketezwa kwa moto katika mzozo wa unaoendelea baina ya maderevawa teksi za kawaida na zile zinazotumia teknolojia ya kisasa kuwatoza wateja wao nauli katika mji mkuu wa kenya-Nairobi.

Hili ni tukio la pili la aina hii katika kipindi cha mwezi mmoja katika jiji la Nairobi.
Mwezi Februari, madereva teksi za kawaida walifanya maandamano jijini Nairobi na walipatia kampuni ya Uber siku saba iwe imesitisha shughuli zake nchini Kenya,baada ya kuishutumu kuvunja sheria za nchi na kuhusika kuwa na ukoloni mamboleo.
No comments:
Post a Comment