Maandamano dhidi ya urushaji wa makombora unaofanywa na Korea Kaskazini
Taifa la Korea Kaskazini limerusha makombora kadhaa ya masafa mafupi katika maji ya pwani yake ya mashariki ,kulingana na kituo cha habari cha Korea Kusini Yonhap.
Washington na Seoul zinafanya mazoezi ya pamoja ya kijeshi huku Korea Kaskazini ikidhania inajiandaa kuivamia.
Korea Kusini ilikuwa ikijaribu kubaini ni aina gani ya makombora yaliohusishwa katika urushaji huo.
Makombora hayo yalidaiwa kurushwa kutoka mji wa Kaskazini Mashariki wa Hamhung.
Siku ya ijumaa Korea Kaskazini ilirusha makombora mawili ya masafa marefu.
Baadaye Marekani iliitaka Pyongyang kutosababisha wasiwasi.

No comments:
Post a Comment