TANGAZO


Thursday, March 24, 2016

Jaji Lubuva: Tumekamilisha uchaguzi mwaka 2015




Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu, Damian Lubuva

Na Jacquiline Mrisho –MAELEZO
Dar es Salaam 24.03.2016

MWENYEKITI wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu, Mhe. Damian Lubuva  amekamilisha uchaguzi wa mwaka 2015 baada ya kumaliza kuteua wabunge wanawake watatu wa viti maalumu waliokuwa wamebakia. 


Uteuzi huo umefanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC na kutangazwa rasmi leo Jijini Dar es salaam na Jaji Mstaafu Lubuva kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi za tume hiyo.


“Tume ya Taifa ya Uchaguzi imewateua ndugu Ritah Kabati na Oliver Semuguruka wa Chama cha Mapinduzi (CCM) na Lucy Owenya wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuwa wabunge wanawake wa viti maalum katika Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.”alisema Lubuva.


Jaji Mstaafu Mhe. Libuva ameongeza kuwa,kwa mwaka 2015 NEC ilitakiwa kuteua wabunge wanawake wa viti maalum 113 ila waliteuliwa jumla ya wabunge 110 ambapo viti vitatu vilibakia kusubiri uchaguzi wa majimbo 8 ambayo uchaguzi wake ulihairishwa kutokana na sababu mbalimbali.


Jaji Mstaafu Lubuva amesema kuwa,NEC hufanya uteuzi wa wabunge wanawake wa viti maalum kutoka kwenye orodha iliyotumwa na Katibu Mkuu wa chama husika hivyo, Tume imewateua wabunge hao kama walivyoorodheshwa kwenye majina yaliyoletwa na makatibu wao.


Hatimaye zoezi la uchaguzi wa mwaka 2015 kwa sehemu zilizosalia  limeisha kwa amani, viongozi waliochaguliwa na kuteuliwa wana wajibu wa kufanya kazi yakuwatumikia wananchi ili kuleta maendeleo kwa Taifa.

No comments:

Post a Comment