TANGAZO


Saturday, February 27, 2016

Mkazi wa Kibamba ajishindia safari ya kwenda Ujerumani na StarTimes

Meneja Uhusiano wa Kampuni ya ving'amuzi ya StarTimes, Muddy Kimwery (kushoto), akishauriana na Mkaguzi wa Michezo ya Kubahatisha nchini, Bakari Maggid kabla ya kuchezeshwa droo ya nne ya Pasua Anga kwa ajili ya kumpata mshindi wa nne kati ya washindi 5 watakaokwenda Ujerumani kuangalia Ligi Kuu ya nchi hiyo, Bundesliga, jijini Dar es Salaam jana. (Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya ving'amuzi ya StarTimes, Muddy Kimwery akibofya kitufe cha kompyuta kuchezesha droo ya nne ya Pasua Anga kwa ajili ya kumpata mshindi wa nne kati ya washindi 5 watakaokwenda Ujerumani kuangalia Ligi Kuu ya nchi hiyo, Bundesliga, jijini Dar es Salaam jana. Kulia anayeangalia ni Mkaguzi wa michezo ya Kubahatisha nchini, Bakari Maggid.
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya ving'amuzi ya StarTimes, Muddy Kimwery akibofya kitufe cha kompyuta kuchezesha droo ya nne ya Pasua Anga kwa ajili ya kumpata mshindi wa nne kati ya washindi 5 watakaokwenda Ujerumani kuangalia Ligi Kuu ya nchi hiyo, Bundesliga, jijini Dar es Salaam jana. Kulia anayeangalia ni Mkaguzi wa michezo ya Kubahatisha nchini, Bakari Maggid.
Meneja Uhusiano wa Kampuni ya ving'amuzi ya StarTimes, Muddy Kimwery akimuonesha namba ya mshindi Mkaguzi wa michezo ya Kubahatisha nchini, Bakari Maggid wakati wa kuchezesha droo ya nne ya Pasua Anga kwa ajili ya kumpata mshindi wa nne kati ya washindi 5 watakaokwenda Ujerumani kuangalia Ligi Kuu ya nchi hiyo, Bundesliga, jijini Dar es Salaam jana.
Mfanyakazi wa Kituo cha Mawasiliano cha Kampuni ya ving'amuzi ya StarTimes, Rehema Luponda akiwasiliana na mshindi wa nne wa droo ya nne wa Pasua Anga, Joseph Mogela (46), mkazi wa Kibamba jijini Dar es Salaam, mara baada ya kuchezeshwa droo hiyo, jijini jana. Kushoto ni Meneja Uhusiano wa kampuni hiyo, Muddy Kimwery na katikati ni Mkaguzi wa michezo ya Kubahatisha nchini, Bakari Maggid.


Dar es Salaam, Februari 26, 2016

IKIWA imebakia droo moja ya bahati nasibu ya kujishindia safari ya kwenda Ujerumani inayoendeshwa na kampuni ya StarTimes Tanzania, mkazi wa Kibamba, Kinondoni jijini Dar es Salaam, Bw. Joseph Mogela (46) ambaye ni dereva katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili amebahatika kuwa mshindi wa nne wa safari hiyo ya kusisimua.


Akizungumza kwa njia ya simu Bw. Mogela alielezea kuwa amefurahi sana kwa kutangazwa huko hasa ukizingatia promosheni hiyo inaelekea ukingoni.

“Nimefurahi sana na nawashukuru StarTimes kwa kunitangaza mimi kuwa mshindi wa droo ya nne ya promosheni hii. Sikutegemea kwa kweli kwa sababu mimi nililipitia kama mteja mwingine ambaye anafurahia huduma za kampuni hii. Lakini nimeshtushwa na simu hii kuwa mimi ndiye mshindi wa droo hii kubwa ambayo ni fursa kubwa sana kwangu mimi.” Alisema Bw. Mogela


“Nashukuru kwa nafasi hii niliyopatiwa ambayo naweza kusema imepatikana kwa mtaji wa kulipia kifurushi cha Mambo kinachopatikana katika king’amuzi cha StarTimes kwa shilingi 12, 000/ tu kwa mwezi. Wakati mwingine sisi wateja huwa tunadharau vitu hivi lakini vinakuwa ni vya kweli, ninaamini mpaka napigiwa simu hii na kuipokea basi bahati ilikuwa ni ya kwangu,” alisema na kumalizia mshindi huyo, “Ningependa kushukuru tena na ninaisubiria hiyo safari kwa hamu kwani kupata fursa ya kwenda Ujerumani kutazama mechi ‘Laivu’ tena bila ya gharama si mchezo. Nawasihi wengine wasipitwe na promosheni hii.”


Naye kwa upande wake Meneja Uhusiano wa kampuni hiyo, Bw. Muddy Kimwery amebainisha kuwa sasa mambo yanakaribia kuiva kwani huyo alipatikana alikuwa ni mshindi wa nne maana yake kwamba amebakia mmoja tu kutangazwa ili kukamilisha idadi ya watano kama tulivyoahidi.


“Leo tumechezesha droo ya nne kwa wateja wetu kujishindia safari ya kwenda Ujerumani kushuhudia mechi ya Bundesliga moja kwa moja uwanjani. Mshindi wetu wa leo anatokea hapahapa Dar es Salaam, anaitwa Joseph Mogela ana umri wa miaka 46 na anafanya kazi ya udereva pale Muhimbili katika Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi. Mshindi huyu anaungana na wengine watatu na amebakia mmoja ambaye tunatarajia wiki ijayo tutampata ili aweze kujumuika na wenzake tayari kwa safari ya pamoja.” Aliongezea Bw. Kimwery


Meneja huyo wa Uhusiano wa Umma kutoka StarTimes alimalizia kwa kusema kuwa, “Najua washindi wetu waliokwishapatikana wana shauku kubwa ya kutaka kujua ni mechi gani watakayoenda kuangalia, lini wataondoka na kurudi. Ningependa kuwatoa hofu, mipango yote inaendelea na tutawafahamisha wote kila kitu kupitia vyombo vya habari kama tulivyofanya kwa kuwaatangaza washindi. Ningependa kuwaambia wajiandae kwani mambo yameanza kuiva, safari inanukia na natoa wito kwa wateja wengine waendelee kulipia na kujiunga na huduma Zetu kwani bado nafasi ni kubwa ya kubahatika na safari hii ya kipekee.”

No comments:

Post a Comment