TANGAZO


Thursday, December 17, 2015

Mhe Kairuki: Ni lazima kufanyakazi kwa ushirikiano Serikalini

Waziri Angella Kairuki.

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais - Utumishi na Utawala Bora Mhe. Angella Kairuki (Mb) ameelekeza ni lazima kufanya kazi kwa ushirikiano Serikalini ili kufikia lengo.

Waziri Kairuki alisema hayo jana katika kikao kazi na Wafanyakazi wa Idara ya Mipango-UTUMISHI.

“ Kufanya kazi kwa ushirikiano ni muhimu ili tufikie malengo tuliyoweka katika Utumishi wa Umma” Mhe. Kairuki alisema na kusisitiza ni jambo lisilopingika kuwa muda mwingi hutumika na Watumishi katika kazi hivyo utamaduni na nidhamu ya kushirikiana ni muhimu ili kuongeza kasi ya kazi na matokeo yasiyokuwa ya kubahatisha.

Mhe. Kairuki alitoa fursa kwa Watumishi wa Umma wenye maoni kuhusu utendaji kazi Serikalini wasikae nayo bali wafike ofisini kwake na kushauri ili wananchi wapate huduma bora zaidi na zenye kiwango kutoka kwa Serikali yao.

Waziri Kairuki alisisitiza kushirikiana kwa karibu na Watumishi nchini ili kuleta maendeleo na kuondokana na mtazamo wa kupokea yanayosemwa na viongozi bila kushauri au kuboresha zaidi.
Mhe. Kairuki ameanzisha utamaduni wa kazi kwa kukutana na Watumishi wa Umma ili kubaini changamoto na kuzifanyia kazi. Wiki hii ameanza na Idara na Vitengo vya ofisi yake.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini


Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora.

No comments:

Post a Comment