Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye na Mbunge wa Viti Maaalum (CCM) Munde Tambwe wakizungumza jambo nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma muda mfupi kabla ya kuanza kwa mkutano wa Bunge hilo leo (Jumatano Novemba 18, 2015).
Mbunge wa Kigoma Kaskazini (CCM), Peter Serukamba (kulia) akibadilishana mawazo na Mbunge wa Busega Raphael Chegeni nje ya ukumbi wa Bunge mjini Dodoma muda mfupi kabla ya kuanza kwa mkutano wa Bunge hilo leo (Jumatano Novemba 18, 2015).
Wabunge wa Viti Maalum (CCM) wakiingia katika ukumbi wa Bunge mjini Dodoma tayari kuanza mkutano wa kwanza wa Bunge hilo leo (Jumatano Novemba 18, 2015.
Mbunge wa Bariadi Magharibi (CCM) Andrew Chenge (kushoto) na Mbunge wa Mwanga (CCM) Prof. Jumanne Maghembe wakiiingia wakiwasili katika viwanja vya Bunge mjini Dodoma tayari kuanza mkutano wa kwanzawa Bunge leo (Jumatano Novemba 18, 2015).
Mbung e wa Viti Maalum kutoka Chama cha Wananchi (CUF) Riziki Saidi Lulida akiapa kiapo cha Uaminifu.
Baadhi ya wabunge wa Chama cha Wananchi (CUF) wakimshangilia mbunge mwenzao Riziki Saidi Lulida bada ya kula kiapo cha Uaminifu.
Mbunge wa Ilala Musa Azan Zungu akiapa.
Mbunge wa Butiama Mhe. Nimrod Mkono akiapa.
Baadhi ya wageni wa wabunge walioapishwa wakiingia na kutoka Bungeni.
Mbunge wa Arumeru Magharibi Joshua Nassari akiapa.
Baadhi ya wabunge wakipata maelekezo kutoka kwa mhudumu wa Bunge (kulia).
Wabunge wa Viti Maalum wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Amina Mollel (kushoto) na Stella Ikupa Alex (kulia) akiwasalimiana na mmoja wa wabunge baada ya kumalizika kwa kikao cha Bunge.
Na Ismail Ngayonga na Lilian Lundo,
Maelezo, Dodoma
17.11.2015
WABUNGE
wa mkutano wa kwanza wa kikao cha kwanza cha Bunge la 11 wamemchagua Job Ndugai (Mb) kuwa Spika wa Bunge la 11 la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.
Ndugai
anakuwa Spika wa 7 wa Bunge la Tanzania tangu uhuru, ambaye alipata kura
254 dhidi ya kura 109 za mshindani wake wa
karibu Goodluck Ole Medeye kutoka Chama Cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA).
Akitangaza
matokeo hayo leo (Jumanne Novemba 17, 2015) msimamizi wa uchaguzi huo ambaye
pia ni Katibu wa Bunge, Thomas Kashilillah alisema jumla ya kura 365 zilipigwa
katika uchaguzi huo, ambapo kura 2
ziliharibika.
Mara
baada ya kuchaguliwa kushika nafasi hiyo, Ndugai alisema ataliongoza Bunge hilo kwa haki
na usawa na hivyo kutoa nafasi kwa Wabunge kutoka vyama vyote vya siasa
kushiriki katika mijadala mbalimbali ndani ya Bunge.
Aidha
Ndugai alisema anafahamu umaskini, mahitaji na matarajio ya Watanzania, kuhusu nafasi ya chombo hicho katika
kuisimamia Serikali, ambayo ni mojawapo ya jukumu la Bunge.
“Namuahidi
Mhe. Rais kuwa Bunge hili litakuwa na ushirikiano na Serikali ya Awamu ya Tano
kwa kusimamia kwa karibu shughuli zote za Serikali ili kunua uchumi wa nchi”
Kwa
mujibu wa Ndugai alisema amepata uzoefu wa nafasi hiyo kutoka kwa Maspika watatu tofauti, ambao ni Pius Msekwa,
Samwel Sitta na Anne Makinda, pamoja na kuongoza kamati mbalimbali za
Bunge, hivyo kupitia uzoefu alioupata
ataweza kufanya kazi hiyo kwa ufansi zaidi.
Kwa
upande mgombea wa nafasi hiyo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA), Goodluck Ole Medeye alisema hatma ya Watanzania ipo mikononi mwa
Bunge hilo, hivyo wabunge hawana budi kutoa ushirikiano kwa Spika ili aweze
kutimiza wajibu wake.
Wakiongea
kwa wakati tofauti, wagombea wengine wa kinyang’anyiro cha nafasi hiyo, walitoa
pongezi kwa Spika Ndugai na kumtaka kulifanya Bunge kuwa chombo chenye
kuwaunganisha Wabunge wote na kuondoa misuguano na tofauti ya vyama ndani ya
Bunge.
Jumla
ya Wagombea 8 kutoka vyama vya AFP, CHADEMA, CCK, NRA, CCM, TLP, CHAUMMA, na
DP waliwania nafasi hiyo, huku mgombea
kutoka CHAUMMA, Hashim Rungwe akishindwa kutoka kufika katika uchaguzi huo
pasipo na kutoa taarifa kwa msimamizi wa Uchaguzi ambaye ni Katibu wa Bunge.
Hata
hivyo Wagombea kutoka katika vyama sita
ambavyo ni AFP, CCK,NRA, TLP, CHAUMMA na DP hawakuweza kupata kura yoyote kati
ya kura halali 363.









No comments:
Post a Comment