Kamishna wa Bajeti kutoka Wizara Fedha Bw. John Cheyo akitoa
ufafanuzi kwa waandishi wa habari leo
jijini Dar es Salaam kuhusu taarifa za upotoshaji zilizoripotiwa na vyombo vya
habari hapa nchini kuwa hazina yakauka, taarifa hizo ni za upotoshaji kwani
mfumo wa Serikali wa bajeti unaiwezesha Serikali kupanga vipaumbele vya matumizi
kulingana na bajeti ilivyopangwa ambapo
fedha zinazokusanywa kupitia mfuko mkuu wa Serikali ndizo hutumika. Kushoto ni
Kamishna msaidizi wa Bajeti Bw. Immanuel Tutuba na kulia ni Mkurugenzi msaidizi
Idara ya habari Maelezo Bw. Vicent Tiganya.
Kamishna wa Bajeti kutoka Wizara Fedha Bw. John Cheyo
akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu kubadilishwa
kwa matumizi ya Fedha za Serikali ambazo zitaelekezwa kwenye shughuli
zitakazowagusa wananchi ikiwemo uboreshaji wa sekta ya elimu ambapo awali fedha
hizo zilipangwa kutumika katika sherehe za Uhuru na shughuli zisizo za lazima.
Kulia ni Mkurugenzi msaidizi Idara ya Habari (Maelezo), Bw. Vicent Tiganya.
Kamishna Msaidizi wa Bajeti, Immanuel Tutuba akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari, Dar es Salaam leo, kuhusu namna Serikali inavyokusanya mapato yake na kuyaingiza katika mfuko mkuu wa serikali ili yaweze kutumika katika utekelezaji wa bajeti yake. Kulia kwake ni Kamishna wa Bajeti, John Cheyo, Msemaji wa Wizara ya Fedha, Ingiahedi Mduma (kushoto) na kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari (Maelezo), Vicent Tiganya.
Baadhi ya Waandishi wa Habari wakifuatilia mkutano wa
Wizara ya Fedha na vyombo vya habari ambapo Kamishna wa Bajeti kutoka Wizara hiyo
Bw. John Cheyo alitoa ufafanuzi kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Serikali
kulingana na mipango iliyowekwa katika kuwahudumia wananchi.
Kamishna msaidizi wa Bajeti Bw.Immanuel Tutuba
akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam .Kulia nia
Msemaji wa Wizara ya Fedha Bi. Ingiahedi Mduma. (Picha zote na Frank Mvungi-
Maelezo)

No comments:
Post a Comment