TANGAZO


Sunday, May 24, 2015

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Kassim Majaliwa azindua rasmi kampeni ya Fistula

Naibu waziri ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)Mh. Kassim Majaliwa (Kulia)akikabidhiwa hundi yanye thamani ya shilingi milioni 100/- na Meneja Biashara Idara ya Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Grace Lyon, kwa niaba ya hospitali ya CCBRT kwa ajili ya kampeni ya kutokomeza Fistula nchini  wakati wa Maadhimisho ya Kimataifa ya Fistula yaliyofanyika  kitaifa  katika Wilaya ya Mbogwe  mkoani Geita mwishoni mwa wiki. Katikati ni Naibu Mkurugenzi wa Hospitali ya CCRBT  Haika Mawala, Maadhimisho hayo hufanyika kila mwaka Mei 23.
Meneja Biashara Idara ya Uhusiano wa Vodacom Tanzania Grace Lyon, akiwasikiliza jambo baadhi ya watoto waliofika na wazazi wao katika maadhimisho  ya Kimataifa yaliyofanyika  kitaifa  katika Wilaya ya Mbogwe  mkoani Geita. Vodacom Foundation ilikabidhi Hundi yenye thamani ya shilingi milioni 100/- Naibu waziri ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mh. Kassim Majaliwa (hayupo pichani) kwa  niaba ya Hospitali ya CCRBT kwa ajili ya kutokomeza fistula nchini, Maadhimisho hayo hufanyika kila mwaka Mei 23. 
 Naibu Mkurugenzi wa Hospitali ya CCRBT  Haika Mawala (kushoto) na  Meneja Biashara Idara ya Uhusiano wa Vodacom Tanzania, Grace Lyon wakimuangalia mtoto  Nyambole  Kulubone mwenye tatizo la  mdomo wa sungura akiwa amebebwa na mama yake Mariam Sanda(22) Mzazi huyo aliyehudhuria katika Maadhimisho ya Kimataifa ya Fistula aliaidiwa na Mkurugenzi wa hospitali ya CCBRT(kushoto) kuwa mtoto huyo atatibiwa bure katika hospitali hiyo wakati walipomuona kwenye Maadhimisho ya   Kimataifa ya Fistula yaliyofanyika  kitaifa  katika Wilaya Mbogwe Geita. Ambapo Taasisi ya Vodacom Foundation ilimkabidhi hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 100/-Naibu waziri ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mh. Kassim Majaliwa (hayupo pichani) kwa  niaba ya Hospitali hiyo kwa ajili ya kutokomeza fistula nchini, Maadhimisho hayo hufanyika kila mwaka Mei 23. 
Naibu waziri ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mh. Kassim Majaliwa (kushoto) akimsisitiza jambo Meneja Biashara Idara ya Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Grace Lyon, wakati wa Maadhimisho ya   Kimataifa ya Fistula yaliyofanyika  kitaifa  katika Wilaya Mbogwe Geita.Meneja huyo alimkabidhi waziri huyo  hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 100/- iliyotolewa na taasisisi ya Vodacom foundation kwa ajili ya kutokomeza fistula nchini. 
Meneja Biashara Idara ya Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Grace Lyon(kushoto) akimsisitizi jambo Balozi wa Fistula nchini Mrisho Mpoto  wakati wa Maadhimisho ya   Kimataifa ya Fistula yaliyofanyika  kitaifa  katika Wilaya Mbogwe Geita mwishoni mwa wiki. Ambapo Taasisi ya Vodacom Foundation ilimkabidhi hundi yenye thamani ya shilingi Milioni 100/- Naibu waziri ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Mh. Kassim Majaliwa(hayupo pichani)kwa  niaba ya Hospitali ya CCBRT kwa ajili ya kutokomeza fistula nchini, Maadhimisho hayo hufanyika kila mwaka Mei 23.

No comments:

Post a Comment