TANGAZO


Wednesday, April 22, 2015

Serikali ya Tanzania na Korea ya Kusini zabadilishana uzoefu katika kuimarisha uwekezaji

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Prof. Adolf Mkenda akifungua kongamano kongamano la siku moja lililofanyika leo jijini Dar es salaam kuhusu masuala ya uwekezaji kati ya Tanzania na Korea ya Kusini ili kubadilishana uzoefu na kushirikiana katika kuinua uchumi wa nchi zote mbili kwa kushirikisha sekta ya Umma na sekta binafsi katika kujiletea maendeleo endelevu. 
Baadhi ya wajummbe kutoka nchini Korea ya Kusini wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Prof. Adolf Mkenda (hayupo pichani) wakati alipokuwa fungua kongamano la siku moja lililofanyika leo jijini Dar es salaam kuhusu masuala ya uwekezaji kati ya Tanzania na Korea ya Kusini ili kubadilishana uzoefu na kushirikiana katika kuinua uchumi wa nchi zote mbili kwa kushirikisha sekta ya Umma na sekta binafsi katika kujiletea maendeleo endelevu. 
Baadhi ya wajummbe kutoka Tanzania wakifuatilia mjadala wakati wa kongamano la siku moja lililofanyika leo jijini Dar es salaam kuhusu masuala ya uwekezaji kati ya Tanzania na Korea ya Kusini ili kubadilishana uzoefu na kushirikiana katika kuinua uchumi wa nchi zote mbili kwa kushirikisha sekta ya Umma na sekta binafsi katika kujiletea maendeleo endelevu. 
Picha ya pamoja ya wajumbe kutoka Tanzania na Korea ya Kusini walioshiriki kongamano la siku moja lililofanyika leo jijini Dar es salaam kuhusu masuala ya uwekezaji ili kubadilishana uzoefu na kushirikiana katika kuinua uchumi wa nchi zote mbili kwa kushirikisha sekta ya Umma na sekta binafsi katika kujiletea maendeleo endelevu. Kutoka kushoto walioketi ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Prof. Adolf Mkenda. (Picha na Wizara ya Fedha)

Na mwandishi wetu.
SERIKALI ya Tanzania na Korea ya Kusini zimefanya kongamano la siku moja kuhusu masuala ya kiuchumi ili kubadilishana uzoefu na kushirikiana katika kuinua uchumi wa nchi zote mbili kwa kushirikisha sekta ya Umma pamoja na sekta binafsi katika kujiletea maendeleo endelevu.

Kauli hiyo imetolewa leo na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Prof. Adolf Mkenda alipokuwa akifungua kongamano hilo lililofanyika leo jijini Dar es salaam.

Kongamano hilo lilikuwa na lengo kuiwezesha Tanzania kujifunza namna ya kuendesha masuala ya bajeti ya nchi na namna ya kushirikisha sekta binafsi na sekta ya Umma katika kuinua uchumi wa nchi.
Prof. Adolf Mkenda alisema kuwa kupitia kongamano hilo Tanzania imejifunza kutoka Korea ya Kusini namna ya kushirikisha sekta binafsi na sekta ya Umma katika kuwaletea wananchi maendeleo endelevu na ya nchi kwa ujumla.

“Kama nchi, tumeona ni vema kujifunza kutoka kwa wenzetu wa Korea ya Kusini ili kupata fursa na uzoefu katika kutoa huduma bora kwa wananchi kwa kuwa Korea ya Kusini ni miongoni mwa nchi zinzoongoza duniani kwa kuwa na uchumi imara walionao kwa kushirikisha sekta binafsi” alisema Prof. Mkenda.

Ili kupata maendeleo endelevu, Prof. Mkenda alisema kuwa jukumu la Serikali ni kushirikiana na sekta binafsi na kujiwekea mikakati mbalimbli itakayosaidia kuibua miradi ambayo itakuwa na ushindani ambapo kwa namna hiyo itasaidia nchi kuwa na maendeleo na hivyo kupata faida na kuinua uchumi wa nchi na kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla.

Aidha, Prof. Mkenda alisema kuwa fursa hiyo ya kushirikisha sekta binafsi imeanza kuwa na mafanikio nchini ambapo tayari Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepisha mswada wa namna ya Serikali kushirikiana na sekta binafsi (PPP) katika kuleta maendeleo nchini.

Kwa upande wake mwakilishi wa Korea ya Kusini Dkt. Cae One Kim aliishukuru Serikali ya Tanzania kwa kuwa na ushirikiano mzuri katika kukuza na kuinua uchumi kati ya nchi hizo mbili ambapo Serikali zote mbili zinaimarisha na kujenga ushirikiano na sekta binafsi katika kujiletea maendeleo.

Dkt. Kim alisema kuwa uhusiano na ushirikiano mzuri uliopo kati ya pande hizo mbili ndiyo umekuwa ni msingi wenye manufaa ambapo utaendelea kukuza sekta za kiuchumi, kibiashara, teknolojia na masuala ya kiutamaduni kati ya nchi hizo.

“Serikali ya Korea imetambua na kuiona Tanzania ni sehemu muhimu katika kukuza mahusiano ya kiuchumi ambayo yatasidia nchi hizi mbili kunufaika, kukuza na kuimarisha uhusiano uliopo baina yetu” alisema Dkt. Kim.

Mahusiano ya kidiplomasia kati ya Tanzania na Korea ya Kusini siyo ya muda mrefu kama ilivyo kwa Korea ya Kaskazini.


Uhusiano huo kihistoria umeanza katika miaka ya 1990 ambapo Korea ya Kusini imekuwa nchi ya matumaini kwa kuwa imepata maendeleo makubwa duniani ambapo Tanzania itaendelea kunufaika na kujifunza ili kuimarisha uchumi wake hasa katika kipindi hiki cha ushindani katika ulimwengu wa sayansi na teknolojia.

No comments:

Post a Comment