TANGAZO


Monday, April 20, 2015

Mkutano wa Kisheria wa 10 wa kundi la Afrika

Waziri wa Fedha  Mhe. Saada Salum Mkuya akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha  na Mlipaji Mkuu wa Serikali  Dr. Servacius Likwelile kushoto kwake kwa pamoja wakifuatilia kwa makini mkutano  wa 10 wa kisheria wa kundi la Afrika (Afrikca Group Constituency) uliokuwa ukiendelea mjini Washington DC.
Waziri wa Fedha  Mhe. Saada Salum Mkuya akiwa na Katibu Mkuu wa kwa pamoja wakifuatilia kwa makini mkutano wa 10 wa kisheria kundi la Afrika (Afrikca Group Constituency) uliokuwa ukiendelea mjini Washington DC.
Waziri wa Fedha  Mhe. Saada Salum Mkuya akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha  na Mlipaji Mkuu wa Serikali  Dr. Servacius Likwelile kushoto kwake kwa pamoja wakifuatilia kwa makini mkutano wa 10 wa kisheria wa kundi la Afrika (Afrikca Group Constituency) uliokuwa ukiendelea mjini Washington DC.
Waziri wa Fedha  Mhe. Saada Salum Mkuya akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha  na Mlipaji Mkuu wa Serikali  Dr. Servacius Likwelile kushoto kwake kwa pamoja wakifuatilia kwa makini mkutano  wa 10 wa kisheria wa  kundi la Afrika (Afrikca Group Constituency) uliokuwa ukiendelea mjini Washington DC.
Waziri wa Fedha  Mhe. Saada Salum Mkuya akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha  na Mlipaji Mkuu wa Serikali  Dr. Servacius Likwelile kushoto kwake kwa pamoja wakifuatilia kwa makini mkutano wa 10 wa kisheria wa kundi la Afrika (Afrikca Group Constituency) uliokuwa ukiendelea mjini Washington DC. 
Waziri wa Fedha  Mhe. Saada Salum Mkuya akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha  na Mlipaji Mkuu wa Serikali  Dr. Servacius Likwelile kushoto wakifuatilia semina iliyokuwa ikitolewa kuhusu uimarishaji wa makazi mijini.
Waziri wa Fedha  Mhe. Saada Salum Mkuya akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha  na Mlipaji Mkuu wa Serikali  Dr. Servacius Likwelile kushoto wakifuatilia semina iliyokuwa ikitolewa kuhusu uimarishaji wa makazi mijini. Aliyeko nyuma ya waziri ni Bw. Ngosha Saidi Magonya, Kamishina wa Fedha za nje.


NCHI ZA AFRIKA ZA TOA MSIMAMO WAO KWA IMF  NA WB
WAKATI Mikutano ya Benki ya Dunia na Shirika la kifedha la kimataifa ikiendelea hapa Mjini Washington Dc. Mawaziri wa fedha wameweka misimamo yao juu ya sera ambazo zinawekwa na Benki ya Dunia.

Akizungumza na vyombo vya habari,waziri wa fedha  wa Tanzania Mhe. Saada Salum Mkuya alisema” Sisi  kama nchi tuliwasilisha nini tunaona katika utekelezaji wa mipango ya Benki. Tumeshukuru sana Benki ya Dunia kwa kuendeleza mipango ya kuweza kusaidia nchi za kiafrika ,hususan kwenye mipango ya kujenga  miundo mbinu ya kiuchumi  kama vile barabara, kilimo pamoja na miundo mbinu ya maji  na umeme”.

“Lakini vilevile tumeonyesha wasiwasi wetu kutokana na sera ambazo Benki ya Dunia imeziweka, kama vile kuangalia sera zile za watu wa kiasili ya kiafrika, sisi tumehisi mbali ya nia nzuri na njema ya Benki hii ya Dunia, lakini inaweza kuwa ni kikwazo kikubwa kwa maendeleo ya nchi zetu  kwa sababu sera hiyo inaweza kutumika kuigawa nchi ambayo misingi yake imekuwa ikijengwa kwa umoja kutoka uhuru”.Alisistiza Mkuya.

Hakuishia hapo aliendelea kutoa mfano kuwa “sisi watanzania tumekuwa wamoja ingawa tuna lugha mbalimbali kutokana na makabila tofauti. Lakini tumekuwa pamoja kwa kipindi cha miaka 50.Kwa hiyo tumeona sera hiyo isije ikatumika kwa ajili ya kuwa kigezo cha utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini.

Sisi kama wa Afrika na viongozi wa Afrika tunashirikiana kuona kuwa sera zinazowekwa hazitukwamishi”.

Hali hii ya kudai uasilia (indigenous) imeibuka zaidi katika miongo hii miwili, wakati kukiwa kumejitokeza watu wanaodai kuwa wao hawatambuliki na hoja  hii inaihusu hasa nchi ya  Tanzania.

Mawaziri wa Fedha kutoka Afrika wamejadili mambo mbali mbali ambapo ni pamoja na masuala ya maendeleo  na mahusiano yao na Benki ya Dunia.

Katika Mkutano huo wa kisheria  Mkurugenzi Mtendaji ndiye ambaye amewasilisha maazimio ya Benki katika kipindi  cha miezi sita.Aliongeza Mkuya.

Aidha katika mkutano huo pia walizungimzia suala la Ebola. “Kwa kweli wamekubali kusaidia nchi zile ambazo zimekumbwa na gonjwa hili lakini wamezitaka nchi za afrika na zenyewe kushirikiana katika kupambana na gonjwa hili”.Alimalizia Mkuya.

Mikutano hiyo bado inaendelea hapa mjini Washington DC. Hali ya hewa ni baridi kiasi.
Imetolewa na Msemaji :Wizara ya fedha
 Ingiahedi C.Mduma
Washington DC

18/04/2015

No comments:

Post a Comment