Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Amos Makalla, akizungumza na watendaji wa wilaya ya Rufiji, watendaji wa mradi wa maji wa Kibiti na wawakilishi wa wananchi kuhusu mradi wa Kibiti.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Amos Makalla akiondoka kwenye ofisi ya Mradi wa Maji wa Kibiti baada ya kufanya mazungumzo.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Amos Makalla akikagua baadhi ya miundombinu ya mradi wa Maji wa Kibiti.
. Mhandisi wa Maji wilaya ya Rufiji, Mhandisi Frobert Andrea (wa pili kushoto) akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Amos Makalla kuhusu mradi wa Jaribu Mpakani wakati alipotembelea mradi huo.Kushoto ni Mbunge wa Kibiti Mhe. Abdul Malombwa.
Baadhi ya wakazi wa Jaribu Mpakani waliohudhuria mkutano wao na Naibu Waziri, wakisikiliza taarifa ya Mradi wao, iliyowasilishwa na Mhandisi Frobert Andrea.
Diwani wa Kata ya Mjawa ulipo mradi wa Maji wa Jaribu Mpakani, Ramadhani Mketo, akizungumza katika mkutano huo.
Mkuu wa Wilaya ya Rufiji, Mhe. Nurdin Babu, akizungumza kwenye mkutano huo.
Mbunge wa Kibiti, Mhe. Abdul Malombwa akimkaribisha Naibu Waziri kuzungumza na wananchi wa Jaribu Mpakani.
Naibu Waziri
wa Maji, Mhe. Amos Makalla akizungumza na wananchi wa Jaribu Mpakani kuhusu
mradi wao.
Naibu Waziri
wa Maji, Mhe. Amos Makalla, akiagana na wenyeji wake kabla ya kuondoka. (Picha zote na Hussein Makame-MAELEZO)
Na Hussein
Makame-MAELEZO
SERIKALI
imeahidi kutoa shilingi Milioni 50 kuboresha mradi wa maji wa Jaribu Mpakani ulioko
wilyani Rufiji mkoani Pwani, kufuatia mradi huo kushindwa kufanya kazi kutokana
na baadhi ya miundombinu yake kushindwa kukidhi mahitaji ya wakazi wa eneo
hilo.
Ahadi hiyo
imetolewa na Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Amos Makalla wakati akizungumza na
wananchi wa Jaribu Mpakani baada ya kutembelea na kukagua miradi ya maji ya
Kibiti na Jaribu Mpakani ambayo imekumbwa na changamoto katika uendeshaji wake.
Akieleza
changamoto za mradi huo, Mhandisi wa Maji wilaya ya Rufiji Mhandisi Frobert
Andrea, alisema mradi huo uliojengwa na Serikali mwaka 2005 kwa Shilingi
Milioni 139,umeshindwa kufanya kazi baada ya mabomba yake kupasuka kutokana na
msukumo mkubwa wa maji.
Alisema baada
ya hapo, Halmashauri ya wilaya ya Rufiji ilitoa shilingi Milioni 24.4 kuchimba
kisima kirefu kipya cha mita 120 na Mbunge kutoa Shilingi Milioni 15 kuboresha
mradi huo, lakini juhudi hizo zilishindwa kuwapatia maji baada ya mabomba
kupasuka.
Kutokana na
changamoto hiyo, mradi huo ulihitaji Shilingi Milioni 50 ili kurekebishwa
mabomba, tenki la maji na vituo vya kutolea maji, fedha ambazo zilishindwa
kupatikana.
Akizungumzia
hali hiyo, Mhe. Naibu Waziri Makalla aIiibua matumaini ya wakazi wa eneo hilo
ambao walionesha kutokuwa na furaha kutokana na kutofanya kazi kwa mradi huo.
“Asubuhi
tulipokutana, nikamuuliza Mkuu wa Wilaya na Mbunge sasa nyinyi mnaomba Milioni
50 wakati Serikali haina fedha nyie mnachangia kiasi gani? wakasema hatuna fedha?”
“Lakini kwa maneno
niliyoyasikia kutoka kwa Katibu Mwenezi wa CCM anavyoimba hapa mpaka anataka kutoa
machozi, na kwa mazungumzo niliyofanya na mbunge wa hapa na kwa sura za kina
mama mbele yangu mimi naridhia kubeba mzigo huu kurudi wizarani wanipe fedha hizi”
alisema Mhe. Makalla na kuongeza:
“Kwa sababu
sisi tumeshatumia shilingi Milioni 139, kwa nini tuzipoteze hizi fedha, kwa
hiyo hizi Milioni 50 ziwe mwendelezo wa
kuboresha huu mradi ambao tulishauanza sio mpya.
“Kwa hiyo
mimi hili nalibeba na hata hapa nimeshafanya maamuzi nimeshamuandikia Mkurugeni
wa Maji Vijijini alipokee na alitekeleze.Nitakwenda kuongea na Waziri na zaidi
Waziri wangu ni mtu mzuri ananiamini na amenipa Mamlaka.
“Mhe.
Maghembe ni mtu na mwalimu mzuri na ana nia nzuri nikimueleza anasema endelea
fanya kazi.Kwa hiyo uamuzi huu umeshakwisha na naamini tutaendelea kushirikiana”.
Mbali na
kutoa ahadi hiyo, Mhe. Waziri Makalla alimuomba Mkuuu wa Wilaya asimamie
uboreshaji huo na kuhakikisha fedha zinatumika kama zilivyokusudiwa hadi senti
tano ya mwisho inayotumika.
“Naomba ufanye hivyo ili watu wa Jaribu Mpakani
wapate maji na ndio maana ya Serikali hii ni sikivu, nimeshakuja Serikali
nimewasikia na nimechukua maamuzi ya haraka” alisema.
Akitoa
shukrani Diwani wa Kata ya Mjawa,Ramadhani Mketo alikiri kwamba wananchi wa
Jaribu Mpakani wamepata majibu tena majibu sahihi kabisa na ametaka uharakishwe
ili wapate maji.
“Kwa hiyo
mimi nimshukuru sana Mhe. Naibu Waziri na nimuombee watu wa Mvomero wampe kura
nyingi na pia nimshukuru Mhe. Mbunge kwa juhudi zake za kuwapatia maendeleo
wananchi.” alisema.
Akiwa katika
Mradi wa Maji wa Kibiti, Naibu Waziri Mhe. Amos Makalla ameshauri kuundwa kwa
Mamlaka ya Maji na Bodi ya Maji ya mradi wa Kibiti ili kukidhi mahitaji ya
uendeshaji wa mradi huo mkubwa wa maji.
Mradi wa
Maji wa Kibiti umekua ukikabiliwa na gharama kubwa za uendeshaji mbali na
changamoto ya kukatika mara kwa mara kwa umeme, hali inayofanya maji kutofikia
wananchi kama inavyotakiwa.
Kufuatia
changamoto hizo, Mhe. Makalla aliomba mchakato uanze wa kuunda vyombo hivyo
viwili kwani anaamini mradi huo ni mkubwa hivyo kamati ya maji inayouendesha
inakosa nguvu ya kuuendesha.
Alisema kuna
haja kwa uongozi wa juu wa Wizara ya Maji na ule wa Wizara ya Nishati na Madini
kukutana ili kujadili jinsi ya kushiriiana na kuhakikisha inaokoa miradi mingi
ya maji inayoshindwa kufanya kazi kwa kukosa umeme.
No comments:
Post a Comment