TANGAZO


Wednesday, January 28, 2015

Vijana wa Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo wahamasika na Elimu ya Ujasiriamali

Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo Bibi Nuru Mwendapole kushoto akizungumza na Mwezeshaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa jana wakati wa ziara ya kutembelea Wilaya hiyo kwa ajili ya kutoa elimu ya Ujasiriamali, Ujuzi, Stadi za Maisha na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana kwa vijana wa Wilaya ya Busokelo Mkoa wa Mbeya.
Mwezeshaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa akiwasisitizia vijana wa Wilaya ya Busokelo umuhimu wa kuijua Sera ya Maendeleo ya Vijana jana wakati wa semina ya Ujasiriamali, Stadi za Maisha, Ujuzi na Mfuko wa Maendeleo ya Vijana iliyofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Busokelo Mkoa wa Mbeya. 
Maafisa kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakimsikiliza kwa makini kijana kutoka kikundi cha Vijana Maendeleo wanaofuga samaki wakati wa ziara ya kutembelea vikundi vya vijana wa Wilaya ya Busokelo Mkoa wa Mbeya.
Samaki wakionekana kwa mbali katika bwawa la samaki linalomilikiwa na kikundi cha Vijana cha Maendeleo kilichopo Wilaya ya Busokelo Mkoa wa Mbeya. 
Kutoka kulia ni Mwezeshaji kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi Ester Riwa, Afisa Vijana Mkoa wa Mbeya Bw. George Mbijima, Afisa Maendeleo ya Vijana Bi. Amina Sanga na Mkuu wa Kituo cha Vijana Sasanda Mbeya Bw. Laurean Masele wakiangalia nguruwe wa kikundi cha Search Group Wilaya ya Busokelo walipowatembelea kuangalia shughuli zinazofanywa na kikundi hicho. (Picha zote na Genofeva Matemu – Maelezo. Busokelo, Mbeya)

No comments:

Post a Comment