TANGAZO


Thursday, January 29, 2015

Bungeni leo: Serikali yaboresha mazingira ya utoaji wa elimu ya watu wazima

Waziri Dk. Kawambwa
Na Lorietha Laurence-Maelezo
SERIKALI imeendelea kuboresha mazingira ya utoaji  wa  Elimu ya watu wazima nchini kote wakiwemo wanawake  kwa  mkoa wa Mwanza  chini ya  sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 .

Akijibu swali la Mbunge wa viti maalum mhe. Leticia Nyerere, kuhusu  asilimia ndogo ya wanawake wasomi kwa mkoa wa Mwanza ukilinganishwa na mkoa wa Kilimanjaro ambapo  Waziri wa Elimu na Mafunzo ya ufundi   Dkt. Shukuru Kawambwa   alieleza tofauti hiyo inatokana na hali ya kiuchumi na kijamii.

Aidha mhe.Kawambwa  ameeleza mpaka sasa serikali imeanzisha pogramu mbalimbali  ikiwemo ya Ndiyo Ninaweza katika wilaya 9 ikiwemo ile ya Ilemela Mwanza,ambapo hutoa mafunzo yake kwa njia ya kieletronic  pamoja na Mpango wa uwiano kati ya Elimu ya Watu Wazima na Jamii ijulikanayo kama  MUKEJA.

“Serikali imechukua hatua mbalimbali kuhakikisha kuwa wananchi wote wakiwemo wanawake wanapata elimu ambayo ni haki yao ya msingi ili kuweza kuwasaidia katika shuguli zao za kila siku za maendeleo” alisema Dkt.Kawambwa.

Aliongeza kuwa ni  jukumu la Wizara, Mikoa na Halmashauri kuhamasisha wananchi kujiunga na program hizo ili kujifunza kuandika,kusoma na kuhesabu kwa manufaa yao na jamii inayowazunguka.

Kulingana na ripoti ya sense ya  watu na makazi ya mwaka 2014  iliyofanyika mwaka 2012 ambapo inaeleza asilimia 24.5 ya wanawake wenye umri wa miaka chini ya 15 na zaidi katika mkoa wa Mwanza hawajui kusoma na kuandika ukilinganisha na mkoa wa Kilimanjaro wenye asilimia 9.7 wakati Dar es Salaam ni asilimia 5.2.

No comments:

Post a Comment