TANGAZO


Monday, December 22, 2014

Waziri Fenella afunga fainali za Copa Coca Cola 2014

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara(MB) akikagua timu za Vijana waliochini ya miaka 15 kutoka Kinondoni na Dodoma ambazo zilishiriki hatua ya fainali katika mashindano ya Copa Coca Cola mwishoni mwa wikiendi katika uwanja wa Krume jijini Dar es Salaam. Ambapa katika fainali hizo kwa upande wanaume toimu kutoka Dodoma iliibuka bingwa wa mashindano hayo kwa kuichapa Kinondoni jumla ya magoli 4 -0, wakati kwa upande wa wanawake Kinondoni ilinyakua ubingwa kuifunga Ilala kwa mikwaju ya penati 2 – 1 baada ya dakika tisni kumaliza kwa sare ya mbili mbili.

Mchezaji wa timu ya mpira wa miguu wanawake kutoka Kinondoni akifunga penati wakati wa fainali za Copa Coca Cola 2014 katika mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam mapema wikiendi hii,  Kinondoni ilinyakua ubingwa kwa kuifunga Ilala mikwaju ya penati 2 – 1 baada ya dakika tisni kumaliza kwa sare ya mbili mbili.

Mashabiki wakifuatilia fainali za Copa Coca Cola 2014, Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam leo.

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenella Mukangara (MB) (wa tatu kutoka kushoto) akifurahia mara baada ya kukabidhi  zawadi ya mchezaji bora wa kike katika mashindano ya Copa Coca Cola kwa Golikipa wa timu ya Kinondoni Zubeda Mohamed (15). Wakwanza kutoka kushoto ni Meneja Masoko wa Coca Cola Bw. Godfrey Njowoka, Rais wa TFF Jamal Malinzi na nyuma ya waziri anayecheka ni Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Leonard Thadeo.

Wachezaji wa timu ya Dodoma wakifurahi baada ya kukabidhiwa zawadi zao za ubingwa wa michuano ya Copa Coca Cola baada ya kuibuka mabingwa wa mashindano hayo kwa mwaka 2014 kwa  mashindano hayo kwa kuichapa Kinondoni jumla ya magoli 4 -0, wakati kwa upande wa wanawake Kinondoni ilinyakua ubingwa kuifunga Ilala kwa mikwaju ya penati 2 – 1 baada ya dakika tisni kumaliza kwa sare ya mbili mbili. (Picha zote na Frank Shija, WHVUM)

No comments:

Post a Comment