TANGAZO


Monday, December 22, 2014

Waandaaji wa Tuzo za filamu nchini washauriwa kuzingatia viwango na ubora wa kazi za wasanii


Katibu wa Bodi ya Filamu Tanzania Bibi. Joyce Fissoo (kushoto) akiwa katika kikao cha majadiliano na kamati ya Maandalizi ya Nyumbani Kiswahili Film Awards yaliyofanyika hivi karibuni ofisini kwake jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi  Nyumbani Kiswahili Film Awards Bw. Fadhil Francis Mfate akichangia hoja wakati wa kikao cha majadiliano kuhusu maandalizi ya Tuzo hizo yaliyofanyika katika ofisi za Bodi ya Filamu hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Mkurugenzi wa Utawala wa Kampuni ya Bao Limited Bw. Joseph Noel na Mjumbe wa Kamati ya maandali ya tuzo hizo Bi. Lucia Joseph.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Tabasamu Film Production Bw. Hamza Shaban akifafanu jambo akizungumza wakati wa majadiliano kuhusu maandalizi ya uandaaji wa tuzo za Nyumbani Kiswahili Film baina ya Bodi ya Filamu na Kamati ya Maandalizi ya tuzo hizo yaliyofanyika hivi karibuni jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment