TANGAZO


Friday, December 26, 2014

Rais Dk. Shein afungua Mashindano ya Riadha

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi wakati aliupowasili katika Uwanja wa Amaan Studium kufungua Mashindano ya Riadha  ya Wilaya kumi za Unguja na Pemba leo. (Picha zote na Ikulu)
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein (katikati) akiwa na Viongozi mbali mbali wakiwepo  Wizara ya Habari,Utalii ,Utamaduni na Michezo katika uwanja wa Amaan Studium alipofika kuyafungua mashindano ya riadha kwa Wilaya kumi (10) za Zanzibar
Baadhi ya Vijana na watoto waliofika katika uwanja wa Amaan Studium wakati wa ufunguzi wa   mashindano ya riadha kwa Wilaya kumi (10) za Zanzibar uliofanywa leo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein.
Wachezaji wa riadha wa wilaya ya wete Pemba wakipita kwa maandamano mbele ya mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein kabla ya kuyafungua mashindano ya mchezo huo kwa Wilaya kumi za Unguja na Pemba leo katika uwanja wa Amaan Studium.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein akipunga mkono kama ishara ya kuyapokea maandamano ya wanariadha wa  Wilaya kumi za Unguja na Pemba leo katika uwanja wa Amaan Studium.
Waamuzi wa mchezo wa Riadha wakipita  kwa maandamano mbele ya mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein kabla ya kuyafungua mashindano ya mchezo huo kwa Wilaya kumi za Unguja na Pemba leo katika Uwanja wa Amaan Stadium.
Baadhi ya Wanachezaji wa mchezo wa riadha wakiwa wamejipanga baada ya kupita kwa maandamano mbele ya mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein alipoyapokea maandamano hayo leo katika uwanja wa Amaan Studium pia wakiwepo Chama cha Watu wenye ulemavu wa viungo (SAD’Z).
Wanachezaji wa mchezo wa riadha wakiwa wamejipanga baada ya kupita kwa maandamano mbele ya mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein alipoyapokea maandamano hayo leo katika uwanja wa Amaan Studium pia wakiwepo Chama cha Watu wenye ulemavu wa viungo (SAD’Z).
Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa Zanzibar (BMTZ), Sharifa Khamis alipomkaribisha mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein kuzungumza na wanamichezo wa mchezo wa Riadha kabla kuzinduz rasmi mashindano ya mchezo huo leo katika uwanja wa Amaan Studium Mjini Unguja.
Mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein alipokuwa akitoa nasaha zake kwa  wanamichezo wa mchezo wa Riadha kabla kuzindua rasmi mashindano ya mchezo huo yaliyoanza  leo katika uwanja wa Amaan Studium Mjini Unguja.
Mgeni rasmi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akipiga bastola juu kuzindua rasmi mashindano ya mchezo wa riadha ya Wilaya kumi za Unguja na Pemba leo katika uwanja wa Amaan Studium Mjini Unguja (kushoto) Naibu wa Waziri wa Habari,Utalii, Utamaduni na Michezo Bi. Hindi Hamad Khamis.



Na Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amepokea gwaride la wanariadha kutoka Wilaya kumi za Zanzibar na kuwataka washiriki vizuri pamoja na waamuzi kutenda haki katika mashindano hayo kwani nia ya Serikali  ya Mapinduzi ya Zanzibar ni kufufua vuguvugu la michezo kama ilivyokuwa hapo siku za nyuma.

Mapokezi hayo ya gwaride la wanariadha wa Zanzibar pamoja na waamuzi wa mashindano hayo ambapo pia liliwashirikisha wanamichezo wenye ulemavu, yaliyofanywa na Dk. Shein yalifanyika katika uwanja wa Amaan mjini Unguja na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Serikali, michezo pamoja na wanamichezo na wananchi.
                                                                                  
Akiwasalimia wanaridha hao mara baada ya kupokea gwaride lao lililopita mbele yake likiongozwa na Brasband kutoka Chuo cha Mafunzo Zanzibar, Dk. Shein aliwataka wanariadha hao washiriki vizuri na washindane kwa amani kama lilivyo jina la uwanja huo wanaoshindania mashindano hayo wa Amaan, ambao uliasisiwa na Rais wa mwanzo wa Zanzibar Marehemu Mzee Abeid Amani Karume.
Dk. Shein alisema kuwa kufanikiwa kwa mashindano hayo na kufanyika kwa vizuri huku waamuzi wakitenda haki kutaendelea kumpa hamasa ili apate kuendelea kuyaunga mkono mashindano hayo ili kufikia malengo ya serikali ya kufufua vuguvugu la michezo nchini.
Aidha, Dk. Shein aliungana na wanamichezo hao pamoja na waamuzi wa mashindano hayo kufuata viapo walivyokula mbele yake kuwa watashindana na kucheza kwa amani bila ya ugomvi na kucheza kwa amani huku waamuzi wakiahidi kutenda haki.

Pamoja na hayo, Dk. Shein alitumia fursa hiyo kutoa shukurani kwa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo,  Baraza la Michezo la Taifa la Zanzibar (BMTZ) pamoja na Wizara zote zilizosaidia kuendesha mashindano hayo.

Mapema wanariadha hao walikula kiapo kuwa watashiriki na kushindana kwa kufuata Sheria za Shirikisho la riadha la Afrika na dunia sambamba na kufuata kanuni zote zinazotawala michezo hiyo ambapo waamuzi nao waliapa kufuata sheria za Kimataifa na kanuni zote bila ya woga wala upendelea wowote huku wakiadidi zaidi kutenda haki.
Pamoja na hayo, Dk. Shein mara baada ya kumaliza kutoa salamu zake hizo kwa wanamichezo hao aliyazindua rasmi mashindano hayo ambayo yanatarajiwa kufanyika kwa muda wa siku mbili  terehe (26-27) Disemba mwaka huu.
Mashindano hayo yameandaliwa na Baraza la Michezo la Taifa Zanzibar (BMTZ) kwa kushirikiana na Chama cha Riadha Zanzibar (ZAAA)  chini ya ufadhili wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein.

Lengo la mashindano hayo ni kuinua mcezho wa riadha Zanzibar kuanzia vijijini, maskulini na maeneo mengine pamoja na kufufua vipaji vya wanariadha kutoka katika sehemu husika kwa lengo la kuviendeleza sambamba na kutekeleza sera ya Michezo Zanzibar.

Aidha,  lengo jengine ni pamoja na kuonesha juhudi binafsi za Dk. Shein katika kutekeleza dhamira yake ya kuona kuwa Zanzibar inarejesha hadhi yake ya asili ya ubingwa katika michezo tofauti.

Mashindano hayo yanawashirikisha wanariadha vijana 250 wa kike na kiume kutoka Wilaya zote kumi za Zanzibar na yatahusisha michezo yote ya riadha ikiwemo kukimbia masafa ya mita 100,200,400,800 na 1500. Pia, kurusha mkuki, kurusha tufe na kurusha kisahani.
Fainali za mashindano hayo zinatarajiwa kufanyika kesho jioni ambapo pia, Dk. Shein anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.


No comments:

Post a Comment