TANGAZO


Saturday, December 27, 2014

Benki ya Posta Tanzania yaendesha mafunzo kwa wajisiriamali wa Tunduma


Picha mbalimbali katika mfunzo kwa wajasiriamali yaliyotolewa na Tanzania Postal Bank (TPB) leo Desemba 22, 2014,ukumbi wa Mtenda Sunset jijini Mbeya.
Washiriki wa mafunzo ya ujasiriamali wakifuatilia mafunzo hayo.
Mwelimishaji kutoka Benki ya Posta Tanzania (TPB), akitoa elimu ya ujasiriamali wakati wa semina hiyo.
Washiriki wa mafunzo ya ujasiriamali wakisikiliza elimu ya ujasiriamali iliyokuwa ikitolewa katika semina hiyo.
Washiriki wa mafunzo ya ujasiriamali wakisikiliza elimu ya ujasiriamali iliyokuwa ikitolewa katika semina hiyo.
Washiriki wa mafunzo ya ujasiriamali wakiwa katika semina yao hiyo leo, jijini Mbeya.
Washiriki wa mafunzo ya ujasiriamali wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maofisa wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), wakati wa semina yao jijini Mbeya leo.
Washiriki wa mafunzo ya ujasiriamali wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maofisa wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), wakati wa semina yao jijini Mbeya leo.
 Washiriki wa mafunzo ya ujasiriamali wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Maofisa wa Benki ya Posta Tanzania (TPB), wakati wa semina yao jijini Mbeya leo.

Na Mwandishi Wetu
BENKI ya Posta Tanzania (TPB), kupitia tawi lake la Tunduma, imetoa semina ya mafunzo kwa wajasiriamali wa Tunduma, Wilaya ya Momba. 
Semina hiyo iliyohudhuriwa na wajasiriamali wapatao mia moja,ililenga kuwaelimisha wafanyabiashara hao kuhusu matumiza mazuri ya huduma za kibenki,hususan mikopo inayotolewa na benki hiyo.
Akifungua semina hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Momba Abiudy Saideya, aliipongeza benki ya Posta kwa kutoa mafunzo hayo ambayo aliamini yatawasaidia wafanyabiashara wa Tunduma kukuza uelewa wa matumizi sahihi ya huduma zinazotolewa na taasisi za fedha.
Alisema kuwa wafanyabiashara ni muhimu wakachukua mikopo ili kukuza mitaji yao na kuongeza uzalishaji,lakini bila kuwa na elimu sahihi juu ya matumizi ya mikopo hiyo faida yake inaweza isipatikane. 
"Nawashauri wafanyabiashara mnaohudhuria semina hii kutimia fursa hii kujadiliana ba benki ya Posta ili mfikie muafaka katikati huduma mnazozitaka". 

Pia aliwaasa wafanyabiashara hao kujiepusha na biashara haramu zitokanazo na bidhaa haramu zilizozagaa mpakani mwa wilaya yao, kwani kwa kufanya hivyo bishara zao zitataifishwa na hivyo kupoteza mitaji yao.

Mkurugenzi wa Mikopo wa benki ya Posta Henry Bwogi iliwasisitiza wafanyabiashara hao kutembelea tawi la benki hiyo lililopo hapo Tunduma, ili kujipatia huduma zote za kibenki hususan mikopo itakayowawezesha kukuza mitaji yao. 

Alisema kuwa benki yake inatoa mikopo ya aina nyingi,kuanzia ile ya vikundi hadi ya wafanyabiashara wakubwa, na riba zinazotozwa na benki hiyo ni za nafuu sana .

No comments:

Post a Comment