TANGAZO


Wednesday, November 12, 2014

Mdahalo wa Matokeo ya Utafiti ya Taasisi ya Twaweza wa maoni ya wananchi ya nani awe Rais 2015? Wafanyika jijini Dar es Salaam

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye (katikati), akichangia wakati wa mdahalo wa matokeo ya utafiti ya Taasisi ya Twaweza wa maoni ya wananchi ya nani awe Rais 2015? Dar es Salaam. Kulia ni Mtafiti Elvis Mushi kutoka taasisi hiyo na Mhadhili wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Benson Bana ambaye pia alikuwa mchangiaji wa mdahalo huo. (Picha zote na Richard Mwaikenda: Kamanda wa Matukio Blog)
Baadhi ya washiriki wakiwa katika mdahalo huo.
Maria Sarungi kutoka Taasisi ya Change Tanzania, akichangia katika mdahalo wa matokeo ya utafiti wa Taasisi ya Twaweza wa maoni ya wananchi ya nani awe Rais 2015.Kushoto ni mmoja wa wachangiaji wa mdahalo huo, Jenerali Ulimwengu na Mkuu wa Taasisi ya Twaweza, Rakesh Rajani.
Mwanasiasa mkongwe, Jenerali Ulimwengu, akichangia katika mdahalo huo, ambapo alisema kuwa ilipaswa utafiti huo ueleze pia kuwa anayetakiwa kuwa Rais amefanikisha jambo gani muhimu katika Taifa.
Mwanafunzi Loyce Gayo, akichangia hoja katika mdahalo huo wa matokeo ya utafiti wa Taasisi ya Twaweza wa maoni ya wananchi ya nani awe Rais 2015?
Mkuu wa Taasisi ya Twaweza, Ramesh Rajani akitoa maelezo kuhusu mafanikio ya matokeo hayo ya utafiti.
Baadhi ya washiriki wa mataifa mbalimbali wakishiriki kwenye madahalo huo.
Wageni waalikwa wakiwa katika mkutano huo.
Mhadhili wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Benson Bana akichangia hoja. Kulia ni Nape wa CCM.
Nape akichangia wakati wa mdahalo huo.
Andrew Mwakalobo akichangia hoja katika mdahalo huo.
Jenerali Ulimwengu akifurahia jambo na Benson Bana baada ya kumalizika kwa mdahalo huo.
Nape akijadiliana jambo na Maria Sarungi.
Juma Mwapachu akijadiliana jambo na Bashe wa CCM.
Nape akizungumza na wanahabari kuhusu matokeo ya utafiti huo.
Nape akifurahia jambo na Absalom Kibanda  Mhariri Mtendaji wa magazeti ya Mtanzania na Rai.
Mtafiti kutoka Taasisi ya Twaweza, Elvis Mushi akiwasilisha matokeo ya utafiti wa maoni ya wananchi ya nani anatakiwa kuwa rais 2015, katika mdahalo uliofanyika jijini Dar es Salaam. katika utafiti huo, Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa aliongoza kwa asilimia 13, akifuatiwa na Waziri Mkuu wa sasa, Mizengo Pinda kwa asilimia 12 na Wiliblod Slaa asilimia 11.
Nape, Kibanda na Bashe wakijadiliana jambo baada ya matokeo hayo kutangazwa

No comments:

Post a Comment