TANGAZO


Thursday, November 27, 2014

Dk. Shein ahutubia mkutano wa Mabalozi wa CCM Kaskazini A Unguja




Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Katibu Mpya wa CCM Kaskazini Unguja Mula Othman Zubeir alipofika katika Hoteli ya Bravo Club Kiwengwa Wilaya ya Kaskazini A Unguja kuzungumza na Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani katika ziara zake za kuimarisha Chama Mkoa wa Kasakazini Unguja leo. (Picha zote na Ikulu)
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi mbali mbali alipofika katika Hoteli ya Bravo Club Kiwengwa Wilaya ya Kaskazini A Unguja kuzungumza na Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani katika ziara zake za kuimarisha Chama Mkoa wa Kasakazini Unguja leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi mbali mbali alipofika katika Hoteli ya Bravo Club Kiwengwa Wilaya ya Kaskazini A kuzungumza na Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani akiwa katika ziara  zake za kuimarisha Chama cha Mapinduzi katika Mkoa wa Kaskazini Unguja. 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein (kulia) akifuatana na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja Meja Mstaafu Juma Kassin Tindwa (kulia) na Mwenyekiti wa CCM Kaskazini Unguja Juma Haji Juma mara  alipowasili katika Hoteli ya Bravo Club Wilaya ya Kaskazini A Unguja kuzungumza na Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani  katika kuimarisha Chama.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein akiingia katika Ukumbi wa Hotel ya Bravo Club Kiwengwa Wilaya ya Kaskazini A Mkoa wa kaskazini Unguja kuzungumza na Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani  katika ziara za kuimarisha Chama cha Mapinduzi CCM.
Baadhi ya Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani katika Wilaya ya Kaskazini A Unguja wakimkaribisha  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein akizungumza na Viongozi hao katika Ukumbi wa  Hotel ya Bravo Club Kiwengwa wilaya ya Kaskazini A Mkoa wa kaskazini Unguja katika  ziara za kuimarisha Chama cha Mapinduzi CCM.
Baadhi ya Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani katika Wilaya ya Mfenesini Kichama wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein akizungumza na Viongozi hao katika Ukumbi wa  Hotel ya Bravo Club Kiwengwa wilaya ya Kaskazini A Mkoa wa kaskazini Unguja katika  ziara za kuimarisha Chama cha Mapinduzi CCM.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein (kushoto) akitia saini kitabu cha wageni alipofika  katika ukumbi wa Hoteli ya Bravo Club Wilaya ya Kaskazini A Unguja kuzungumza na Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani  katika kuimarisha Chama (kulia) Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai na (kushoto) Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kaskazini A Ali Makame Khamis.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein akiteta jambo na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai (kulia) wakati wa mkutano wa maalum wa kuimarisha Chama cha Mapinduzi CCM kwa  Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani Wilaya ya Kaskazini A Mkoa wa Kaskazini Unguja leo.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein (katikati), Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali Vuai (kulia) Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kaskazini A Ali Makame Khamis  wakiwa katika ukumbi wa  Hoteli ya Bravo Club Wilaya ya Kaskazini A Unguja kuzungumza na Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani  katika kuimarisha Chama.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi pia Makamo Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein akizungumza na Mabalozi na Wenyeviti wa Maskani  katika ukumbi wa Hotel ya Bravo Club Kiwengwa wilaya ya Kaskazini A Mkoa wa kaskazini Unguja katika  ziara za kuimarisha Chama cha Mapinduzi CCM.

Na Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar
RAIS  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein amesema kuwa CCM itaendelea kuyalinda Mapinduzi matukufu ya Januari 12, 1964 pamoja na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa maslahi ya wananchi wote wa Tanzania.
Hayo aliyasema leo, katika Mkutano kati yake na viongozi wa Mashina na Maskani za CCM Wilaya ya Kaskazini A Unguja, Mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya ya Bravo Kiwengwa, Wilaya ya Kaskazini A Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Katika hotuba yake kwa viongozi hao Dk. Shein alisema kuwa kuna kila sababu ya kuyaendeleza na kuyalinda Mapinduzi pamoja na Muungano uliopo kama zilivyofanya awamu zote zilizopita kwani hizo ndio ngao za nchi hii.

Alisisitiza kuwa hakuna mabadala wa Muungano wala Mapinduzi ya Januari 12,1964 na kuwataka viongozi hao kuhakikisha wanazilinda ngao hizo kwa maslahi ya wananchi wote wa Tanzania.
Aidha, Dk. Shein aliwashangaa wale wote wanaotaka kurejesha Katiba ya mwaka 1963 ambayo ni katiba ya Mkoloni na ambayo ilikuwepo kwa maslahi ya Sultani na si kwa Wazanzibari ambao ndio waliokuwa wenye nchi.
Sambamba na hayo, Dk. Shein aliwataka wanaCCM pamoja na Mashekhe wa Mkoa huo kujibu hoja kwa ustarabu hasa zile zinazoletwa kwa visingizio vya kidini huku zikichanganywa na siasa na kusisitiza kuwa si jambo la busara kugombanisha watu kwa kisingizio cha dini.
Alisisitiza kuwa siasa na dini ni vitu viwili tofauti wala siasa sio vurugu na kuwasifu wanaCCM wa Kaskazini kwa juhudi zao hasa kwa historia yao ya ukombozi wa Zanzibar na ndio maana wamekuwa hawatetereki.
Dk. Shein pia, aliwaeleza viongozi hao kuwa chama hicho kinawajali na kinawathamini smbamba na kutambua juhudi zao na kuwahakikishia kuwa kitaendelea kuwanga mkono na kushirikiana nao kwa kutambua umuhimu wao huku akiwaeleza jukumu la CCM ni kuimarisha amani na utulivu nchini.

Katika suala zima la ujenzi wa miundombinu ya barabara Dk. Shein alieleza kuwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imefanya juhudi ya kuagiza vifaa vya ujenzi wa barabara ili kutatua tatizo la miundombinu hiyo kwani tatizo kubwa hivi sasa ni kuwepo kwa uhaba wa vifaa hivyo hapa nchini.
Aidha, Dk. Shein alieleza kuwa tatizo la maji katika eneo la Kijini litatafutiwa ufumbuzi wa haraka pamoja na maeneo mengine sambamba na kutafutiwa ufumbuzi changamoto nyengine zinazowakabili wananchi wa maeneo hayo.

Nae Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai alieleza kuwa wapinzani hawataki Muungano wa aina yeyote na wamekuwa wakitoa visingizio visivyo na msingi na hivi sasa wameamua kuunga mkono Katiba ya Mkoloni ya mwaka 1963 ambayo hivi karibuni katika kongamano lao waliisifu kwa kudai itawasaidia Wazanzibari.
Vuai alisema mtu mwenye akili hawezi kuisifu Katiba ya mwaka 1963 kwani katika hiyo katika kifungu cha 3, inamtambua Sultani kuwa ndie Mkuu wa nchi na Mawaziri wote anawachagua yeye kuendesha Serikali, na kwa mujibu wa Katiba hiyo atarithiwa na vizazi hatua ambayo ndio iliyowafanya wazee wakati huo kufanya Mapinduzi.
Naibu Katibu Mkuu huyo alisema kuwa kama kuna mambo ambayo Wazanzibari wanafaidika nayo ni pamoja fursa iliyopo katika elimu ya juu kupitia Bodi ya mikopo ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na ile ya Zanzibar na kueleza kuwa jambo hilo limo kwenye Katiba inayopendekezwa kwani Wazanzibari wamekuwa wakipata fursa zote mbili za kupata mikopo hiyo.
“Kati ya mwaka 2012 na 2013 vijana wa Kizanzibari wapatao 860  walipata mkopo katika Bodi ya Mikopo ya Zanzibar ba kwa upande wa Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania vijana 1024 wa Kizanzibari walipata mkopo, je hapo utasema Muungano hauna faida.. hakuna sababu kwa vijana hasa wasomi kutoiunga mkono Katiba inayopendekezwa”alisema Vuai.
Aidha, viongozi hao wa Wilaya ya Kaskazini A walitoa pongezi kwa Dk. Shein kwa kusimamia amani na usalama hasa pale kulipojitokeza kikundi cha dini na kujiingiza kwenye siasa kikiwa na azma ya kutaka kuvuruga amani iliyopo nchini.

Katika risala yao viongozi hao walieleza furaha yao waliyonayo kutokana na  juhudi za Dk. Shein katika utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi wa CCM ya mwaka 2010-2015 katika maendeleo kwenye sekta mbali mbali ikiwa ni pamoja na kukamilika kwa skuli za Sekondari za Matemwe na Chaani ambazo tayari zimekamilika na hivi sasa zinatoa huduma.
Viongozi hao walieleza kuwa Hospitali ya Kivunge imepanuliwa na huduma nyingi sasa zinatolewa na  na kituo cha afya kilichopo Pwanimchangani tayari kimeshafunguliwa na kusisitiza kuwa mradi mkubwa wa usambazaji maji kwenda Nungwi kupitia Matemwe na Kijini unaendelea vizuri na hivi karibuni mradi huo unatarajiwa kukamilika.
Aidha, kupitia kwa Dk. Shein viongozi hao walitoa shukurani za dhati kwa Mama Mwanamwema Shein kwa kushirikiana na Mama Asha Suleiman Idd na baadhi ya wake wa Wabunge na Wawakilishi wa CCM kwa kuanzisha na kuendeleza Umoja wao wenye azma ya kuimarisha Chama sambamba na kuwaendeleza akina mama katika vikundi vya uzalishaji mali pamoja na madrasa.
Pamoja na hayo, viongozi hao walieleza haja ya kufanywa taratibu ili somo la historia lisomeshwe kuanzia skuli za msingi  kwani vijana walio wengi hawaifahamu  historia ya nchi yao jambo ambalo  linawaburuza vijana kushawishiwa kirahisi na kujiingiza katika makundi yasiokuwa na faida.

No comments:

Post a Comment