TANGAZO


Sunday, October 5, 2014

Mtemvu mgeni rasmi ugawaji nyama iliyotolewa na Shirika la Misaada la Kimataifa la Kiislamu (IIRO) la Ufalme wa Saud Arabia

Wananchi wa Tandika, Jimbo la Temeke, wakimsikiliza Mbunge wao, Abbas Mtemvu (hayupo pichani), ambaye alikuwa mgeni rasmi katika ugawaji wa nyama ya Sadaka iliyotolewa na Taasisi ya International Islamic Relief Organisation (IIRO) la Ufalme ya Saud Arabia, wakati akizungumza katika hafla hiyo, kwenye kituo cha yatima cha Dar-Al-Arqam Tandika jimboni humo leo. (Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Akinamama wa Tandika, Jimbo la Temeke, wakimsikiliza Mbunge wao, Abbas Mtemvu (hayupo pichani), ambaye alikuwa mgeni rasmi katika ugawaji wa nyama ya sadaka iliyotolewa na Taasisi ya International Islamic Relief Organisation (IIRO) ya Ufalme wa Saud Arabia, wakati akizungumza katika hafla hiyo, kwenye kituo cha yatima cha Dar-Al-Arqam, Tandika jimboni humo leo.
Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu, akizungumza wakati wa hafla ya kugawa nyama ya Sadaka, iliyotolewa na Taasisi ya International Islamic Relief Organisation (IIRO) ya Ufalme wa Saud Arabia, ambapo alikuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo, iliyofanyika kwenye Kituo cha yatima cha Dar-Al-Arqam Tandika jimboni humo leo. Kushoto ni Mkurugenzi wa IIRO, Dk. Mohammed Ali Ibrahim Bokhari na kulia ni Mwakilishi wa shirika hilo, jijini Jeddah, Saudi Arabia, Imad Mursi. 
Mgeni rasmi katika hafla ya ugawaji nyama ya sadaka, Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu, akizungumza wakati wa hafla ya ugawaji nyama hiyo, iliyotolewa na Taasisi ya International Islamic Relief Organisation (IIRO) ya Ufalme wa Saud Arabia, hafla iliyofanyika kwenye Kituo cha yatima cha Dar-Al-Arqam, Tandika jimboni humo leo. 
Katibu wa Taasisi ya International Islamic Relief Organisation (IIRO) ya Ufalme wa Saud Arabia, Ofisi ya Tanzania, Omar Ali Khama (kushoto), akizungumza wakati wa hafla hiyo. Wapili kulia ni Mgeni rasmi katika hafla hiyo, Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu.
Mkurugenzi wa IIRO, nchini Tanzania, Dk. Mohammed Ali Ibrahim Bokhari, akizungumza wakati wa hafla ya ugawaji wa nyama ya sadaka iliyotolewa na taasisi hiyo, Tandika jijini Dar es Salaam leo. Katikati Mgeni rasmi katika hafla hiyo, Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu na kulia ni Mwakilishi wa shirika hilo, jijini Jeddah, Saudi Arabia, Imad Mursi. 
Wafanyakazi wa taasisi hiyo, wakikata nyama tayari kwa kukabidhiwa wananchi na yatima wa kituo hicho, cha Dar-Al-Arqam, Tandika jimboni humo.
Mwakilishi wa shirika hilo, jijini Jeddah, Saudi Arabia, Imad Mursi, akizungumza wakati wa hafla hiyo, Tandika leo.
 Yatima wa Kituo cha Dar-Al-Arqam, Tandika, Jimbo la Temeke, wakiwa katika hafla hiyo. 
Yatima wa kituo cha Dar-Al-Arqam Tandika, Jimbo la Temeke, wakiwa katika hafla hiyo.
Mgeni rasmi katika hafla hiyo, Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu (kulia), akiwa na Mkurugenzi wa IIRO, nchini Tanzania, Dk. Mohammed Ali Ibrahim Bokhari, wakifurahia jambo wakati wa hafla ya kugawa nyama hiyo leo. 
Bango la Taasisi hiyo likiwa kwenye kituo hicho cha yatima, ambacho ni moja ya kituo kinacho hudumiwa na taasisi hiyo.
Waandaaji wakikata nyama hiyo kwa ajili ya kuwagawia wananchi wa Tandika, jimboni Temeke.
Waandaaji wakikata nyama hiyo kwa ajili ya kuwagawia wananchi wa Tandika, jimbo la Temeke.
Mgeni rasmi katika hafla ya ugawaji nyama ya sadaka, Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu, akizungumza wakati wa hafla ya ugawaji nyama hiyo, iliyotolewa na Taasisi ya International Islamic Relief Organisation (IIRO) ya Ufalme wa Saud Arabia, kwenye Kituo cha yatima cha Dar-Al-Arqam, Tandika.
Mgeni rasmi katika hafla ya kugawa nyama ya Sadaka iliyotolewa na Taasisi ya Islamic International Org. (IIRO), Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu, akimpatia nyama hiyo, Nuru Athuman. Kushoto ni Mkurugenzi wa IIRO, nchini Tanzania, Dk. Mohammed Ali Ibrahim Bokhari.
Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu (kushoto), akimkabidhi mkazi wa Tandika Maghorofani, Dotto Athuman, nyama iliyotolewa na Shirika la Kiislamu la Kimataifa (IIRO), kwa ajili ya kitoweo, kuadhimisha Sikukuu ya Idd El Hajj, Dar es Salaam leo. Katikati ni Mwakilishi wa shirika hilo, jijini Jeddah, Saudi Arabia, Imad Mursi.
Mbunge wa Jimbo la Temeke, Abbas Mtemvu (kushoto), akimkabidhi yatima Haidar Said wa Kituo cha yatima cha Dar-Al-Arqam, nyama iliyotolewa na Shirika la Kiislamu la Kimataifa (IIRO), kwa ajili ya kitoweo, kuadhimisha Sikukuu ya Idd El Hajj, Dar es Salaam leo. Katikati ni Mwakilishi wa shirika hilo, jijini Jeddah, Saudi Arabia, Imad Mursi.

No comments:

Post a Comment