TANGAZO


Friday, October 3, 2014

Kinana aingia Pangani kuanza ziara ya kuimarisha Chama Tanga Mjini

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana (katikati) na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, wakitoka kwenye pantoni ya Mv Pangani, baada ya kuvuka kuingia Mjini Pangani tayari kuanza ziara Wilaya ya Tanga Mjini, ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake mkoani Tanga ya kuimarisha uhai wa chama na kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2010.
Kinana akisalimiana na wananchi mjini Pangani, ambapo aliwataka viongozi wa Chama na Serikali kuacha tabia ya kuuza mashamba na ufujaji wa mali.
 Kinana akisalimiana na wananchi mjini Pangani alipokuwa akielekea Tanga Mjini
 Kinana akizungumza na wananchi aliposimama kwa muda katika eneo la Feri mjini Pangani
 Kinana akisoma taarifa fupi aliyopewa na wananchi wa Kijiji cha Kigombe ambapo wananchi waliusimamisha msafara wake ili wasikilizwe kero zao.
 Wananchi wakishangilia baada ya Katibu Mkuu wa CCM, Kinana kuwasili katika Kata ya Marungu kushiriki ujenzi wa jengo la CCM la kata hiyo.
 Kinana akiwasalimia wananchi baada ya kuwasili katika Kata ya Marungu, Tanga.
 Wanachi wakifurahi kumuona Kinana alipowasili katika Kata ya Marungu
 Wasanii wa kikundi cha Tanga All Stars Limited, wakitumbuiza wakati wa mapokezi katika Kata ya Marungu.
 Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Halima Tendegu akihutubia katika Kata ya Marungu
 Diwani wa Kata ya Marungu, Bakari Mambeya akimkabidhi kamba Katibu Mkuu wa CCM, Kinana ikiwa ni ishara ya kumpatia zawadi ya ng'ombe iliyotolewa na wananchi wa kata hiyo.
 Wananchi wakimsikiliza Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye (katikati) alipohutubia katika Kata ya Marungu.

 Waliokuwa wanachama wa vyama vya upinzani, wakionesha kadi zao kabla ya kumkabidhi Kinana aliyewapatia kadi za CCM walipojiunga nacho katika Kata ya Marungu, Tanga.
Waliotoka upinzani wakimkabidhi kadi walipotangaza kujiunga na CCM katika mkutano uliofanyika katika Kata ya Marungu.
 Kinana akionesha kadi lukuki alizokabidhiwa na waliotoka upinzani na kujiunga na CCM katika mkutano wa hadhara Kata ya Marungu.
 Kinana akishiriki kuelezeka bati katika jengo la CCM Kata ya Marungu
 Kinana akiwasalimia wauguzi wa Zahanati ya Machui, alipokwenda kushiriki ujenzi wa nyumba ya mganga wa zahanati hiyo.
 Kinana akishiriki ujenzi wa nyumba yamganaga wa Zahanati ya Machui, wilayani Tanga
Wajumbe wakiwa katika mkutano wa Halmashauri Kuu ya Wilaya ya Tanga, uliohutubiwaq na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.

No comments:

Post a Comment