Makamu wa Rais Dk. Mohemed Gharib Bilali akiwa kwenye picha ya pamoja na Waziri wa Afya na ustawi wa Jamii Dk Seif Rashid leo Jijini Dar es salaam wakati wa Kongamano la wadau wa Sekta ya Afya lililofanyika leo Jijini Dar es salaam. (Picha zote na Frank Mvungi-MAELEZO_Dar es Salaam)
Baadhi ya Wadau wa Kongamano la wadau wa Sekta ya Afya wakiwa wanamsikiliza mgeni rasmi ambaye ni makamu wa Rais Dk. Mohamed Gharib Bilali (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo leo jijini Dar es Salaam.
Na Frank Mvungi-MAELEZO
SERIKALI imesema itaendelea kuboresha huduma za afya hapa
nchini kuanzia ngazi ya Zahanati hadi Hosipitali
za Rufaa zote nchini ili kuhakikisha wananchi wanapata matatibu bora na
yanayoridhisha.
Kauli hiyo imetolewa leo
jijini Dar es salaam na Makamu wa Rais Dkt. Mohamed Gharib Bilali wakati
akifungua Kongamano la wadau wa Afya nchini.
Amesema kuwa Serikali inayo dhamira ya dhati katika
kuhakikisha kuwa kila Mtanzania anapata huduma bora za afya ili apate muda
mzuri wa kuchangia shughuli nyingine za maendeleo akiwa mzima.
Dkt. Bilali ameongeza kuwa Serikali itaendelea kutoa motisha
kwa watumishi wa Sekta ya afya ili waendelee kutoa huduma bora za afya kwa wananchi.
Kwa upande wake Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif
Rashid amesema Tanzania ni moja kati ya nchi nne barani Afrika zilizoweza
kufikia lengo namba 4 la malengo ya millennia katika utoaji wa huduma bora za
afya.
Amesema kuwa hatua imefikiwa baada ya Wizara hiyo kuamua kuanzisha idara maalum itakayohusika kuangalia
ubora wa huduma zinazotolewa hapa nchini ili kuongeza tija katika Sekta ya Afya
kwa kuwapa Wananchi huduma bora zinazokidhi vigezo.
Ameongeza kuwa kwa wale wanaofanya vizuri katika kutoa huduma
za Afya watatambuliwa kwa mchango wao katika kutoa huduma bora.
Dkt. Rashid ametaja vigezo vinavyotumika katika kuwapata
watoa huduma za afya kuwa ni kutoa huduma inavyotakiwa,kutumia utaalamu sahihi
katika kutoa huduma hiyo na kuzingatia viwango vilivyowekwa katika kutoa huduma
za afya.
Aidha Dkt. Rashid ametoa
wito kwa wananchi kujiunga na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) ili waweze
kunufaika na huduma zinazotolewa kupitia
mfuko huo kwa lengo la kuhakikisha wananchi wote wanapata huduma bora za afya.
Kongamano la wadau wa
Sekta ya Afya limehusisha wadau zaidi ya 300 kutoka katika Taasisi
mbalimbali za Serikali na zisizo za Kiserikali na linafanyika kwa muda wa siku
mbili ambapo baadhi ya wadau walitambuliwa kwa kutoa huduma bora za Afya ni
kama vile Hosipitali ya Rufaa Mbeya,KCMC,
na Bugando.
No comments:
Post a Comment