TANGAZO


Monday, August 4, 2014

Vijana wa Halmashauri ya Wilaya ya Nchemba Wapigwa msasa kuhusu Mikopo kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nchemba Mkoani Dodoma Bw. Boniface Mandi akiongea na Timu ya Maafisa Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo  kabla ya kufungua Mafunzo ya Vijana wa Wilaya  hiyo kuhusu Mikopo kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana, kulia ni Afisa Vijana Bi Amina Sanga.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nchemba Mkoani Dodoma Bw. Boniface Mandi akifungua  Mafunzo  ya Vikundi vya Vijana wa Halmashauri ya Wilaya ya Nchemba kuhusu Mikopo kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana.Mafunzo hayo yanatolewa na kuratibiwa na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Vijana wa Wilaya ya Nchemba Mkoani Dodoma wakimsiliza mwezeshaji (hayupo pichani) Bi. Amina Sanga katika Mafunzo ya Vijana wa Halmashauri ya Wilaya hiyo kuhusu Mikopo kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Vijana
Ofisa wa Idara ya Maendeleo ya Vijana kutoka Wizara ya Habari,Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Amina Sanga akimkabidhi Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nchemba Mkoani Dodoma Sera ya Taifa ya Maendeleo.

No comments:

Post a Comment