TANGAZO


Wednesday, May 28, 2014

Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana alakiwa na Sumaye, Nagu wilayani Hanang

* Viongozi wa Chadema wabanwa kwa kuficha Mkataba wa Malipo ya Mnara wa Vodacom



Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akilakiwa kwa furaha na Waziri Mkuu  msitaafu, Frederick Sumaye  alipowasili katika Kijiji cha Mwahu wilayani Hanang, tayari kuanza zira katikaManyara baada ya kumaliza ziara Mkoa wa Singida.Lengo la ziara hiyo ambayo pia ameifanya mkoani Tabora ni kuimarisha uhai wa chama, kukagua, kuhimiza na kusukuma ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa kwa kufuata Ilani ya CCM, kukagua maandalizi ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na kusikiliza kero za Wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.
 Wananchi wakiwa mpakani mwa Mkoa wa Manyara na na Singida wakati wa mapokezi ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana alipokuwa akianza ziara Mkoa wa Manyara.
Kinana akiwa na Sumaye huku wakiwa wamezingirwa na vijana wa kabila la Wabarbaig walipowasili katika Kijiji cha Mahu, Hanang.
Wasichana wa kabila la Wabarbaig, wakishiriki katika mapokezi ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana katika Kijiji cha Mwahu, Hanang.
Wananchi wakisikiliza kwa makini wakati Kinana akihutubia mjini Rndasak, wilayani Hanang.
Wananchi wa Kijiji cha Gidika, wilayani Hanang wakiuzuia msafara wa Kinana ili watoe malalamiko yao ya viongozi wa kijiji hicho kuuza shamba lao lenye heka 612 bila ridhaa yao. Kinana alii taka Serikali ya Wilaya na Mkoa kuhakikisha suala hilo linamalizwa haraka  ili wananchi warudishiwe shamba hilo.

 .Kinana na Nape wakimhoji vizuri Mwenyekiti wa Chadema wa Wilaya ya Hanang, Augustino Mayumba aeleze alikopeleka hati ya mkataba wa mnara wa simu wa Vodacom uliowekwa katika Kijiji cha Basouto ambao alishiriki kutia saini ambapo hadi sasa malipo ya fedha hizo haijulikani nani analipwa. 
Hatua hiyo ya kumhoji ilifikiwa baada Kiongozi huyo kuuliza swali kwenye mkutano wa hadhara wa CCM uliofanyika kwenye Kijiji cha Basouto kuwa viongozi wa CCM wanakula fedha za malipo ya mnara huo uliowekwa eneo la soko. Kinana alimtaka Mayumba aeleze mkataba huo ameuweka wapi. Licha ya kiongozi huyo wa Chadema kukiri kushiriki kusaini mkataba huo lakini alishindwa kueleza kwa kusema kuwa na yeye hajui mkataba huo ulipo, jambo ambalo liliwafanya wananchi kuanza kumzomea. Kinana aliwataka wananchi na serikali kumbana Mayumba hadi aeleze alipouweka mkataba iliserikali ya Kijiji iwe inapata malipo hayo.

Sumaye ambaye pia aliwahi kuwa mbunge wa Jimbo la Hanang, akihutubia katika moja ya mikutano aliyoifanya Kinana wilayani Hanang.
 Kinana akishiriki kusomba mawe kwa ajili ya kujengea sakafu jengo la CCM katika Kata ya Qaloda, wilayani Hanang. PICHA ZOTE NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akihutubia katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Katesh, Hanang.
Mmoja wa wanachama lukuki walioambua kuachana na chama hicho na kujiunga na CCM akionesha kadi ya Cahdema kabla ya kukabidhiwa kadi ya CCM katika  mkutano wa hadhara mjini Katesh, Hanang.

Kinana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye  wakisaidia kupaua katika jengo la maabara la Shule ya Sekondari ya Mwahu walipoanza zira wilayani Hanang, Mkoa wa Manyara.
Kinana akuhutubia katika Kata ya Basouto wilayani Hanang, Manyara.
Kinana akipiga mpira kufunga bao ikiwa ni ishara uzinduzi wa michuano ya soka kwa vijana Endasak, wilayani Hanang, ambapo Mbunge wa Jimbo la Hanang, Dk. Mary Nagu alizizawadia timu zitakazoshiriki mipira na jezi.
Wanamichezo wakimshukuru Mbunge wa Jimbo la Hanang, Dk. Mary Nagu na Kinana  baada ya kukabidhiwa zawadi ya mipira na jezi wakati wa mkutano wa hadhara mjini Katesh, Hanang.
Msichana wa kibarbaig akicheza ngoma wakati wamapokezi ya Kinana wilayani Hanang

No comments:

Post a Comment