Kamishna wa Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka, Hajjat Amina Mrisho, akizungumza katika moja ya mikutano yake na
waandishi wa habari, jijini Dar es Salaam.
UZINDUZI
wa chapisho la Tatu la Taarifa za Msingi za Kidemografia, Kijamii na kiuchumi
linalotokana na Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 (Basic Demographic and
Socio-Economic Profile) katika ngazi ya Taifa uliokuwa umepangwa kufanyika siku
ya Ijumapili tarehe 25 Mei, 2014 umeahirishwa.
Uzinduzi
huo sasa utafanyika rasmi tarehe 10 Juni, 2014 katika ukumbi wa Kimataifa wa
Mikutano wa Mwl. Julius Nyerere uliopo mtaa wa Shaaban Robert jijini Dar es
Salaam kuanzia saa 3:00 asubuhi.
Mgeni
rasmi katika uzinduzi huo atakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.
Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
Aidha,
uzinduzi huo unatarajiwa kuhudhuriwa na watu wapatao mia tano (500) ambao ni
pamoja na Viongozi mbalimbali wa ngazi za juu Serikalini, Mabalozi, Wadau wa
Maendeleo, Viongozi wa Dini, Viongozi wa Vyama vya Siasa, Wawakilishi wa Mashirika
yasiyo ya Serikali na Wadau wa Takwimu nchini.
Kwa
kifupi chapisho hili linatoa viashiria mbalimbali ambavyo ni pamoja na Kiwango cha
uzazi, umri wa kuishi wa mtanzania, vifo vya watoto wachanga, kiwango cha vifo
vya wakina mama vitokanavyo na uzazi na taarifa nyingine kwa ajili ya kupanga
mipango ya maendeleo.
Chapisho
hili ni mwendelezo wa machapisho mbalimbali yanayotolewa na Ofisi zetu mbili
yaani Ofisi ya Taifa ya Takwimu na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Zanzibar
kama ilivyoainishwa kwenye kalenda ya machapisho ya Sensa ya Watu na Makazi ya
mwaka 2012.
Imetolewa na Hajjat Amina Mrisho Said
Kamishna wa Sensa ya Watu na Makazi, 2012
23 Mei, 2014
No comments:
Post a Comment