TANGAZO


Thursday, April 24, 2014

Wananchi wahamasishwa kutumia matofali yanayofungamana, ya Udongo saruji

Mhandisi wa Ujenzi toka Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Vifaa vya Ujenzi na nyumba bora (NHBRA) Bw. John Twimanye akiwaeleza waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu matofali yanayofungamana, ya udongo saruji yanayosaidia kupunguza gharama za ujenzi, wakati wa Mkutano uliofanyika leo, Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO). Kulia ni Fundi Sanifu  wa Wakala Huo, Bw. Allen Wangoma.
Ofisa Habari toka Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Vifaa vya Ujenzi na Nyumba Bora (NHBRA), Bw. Frimin Lyakurwa  akiwaeleza waandishi wa Habari (hawapo pichani) wakati wa Mkutano uliofanyika leo Katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO).

Na Mwandishi wetu
WANANCHI wamehamasishwa kutumia matofali yanayofungamana, ya udongo saruji ili kupunguza gharama za ujenzi.

Hayo yamesemwa na Mhandisi wa Ujenzi toka Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Vifaa vya Ujenzi na nyumba bora (NHBRA) Bw. John Twimanye wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam.

Mhandisi Twimanye alisema Matofali hayo yanasaidia kupunguza gharama za ujenzi kwa asilimia 30 ukilinganisha na matofali ya kawaida ya Mchanga.

“Matofali ya udongo saruji yanapunguza gharama za ujenzi kuanzia hatua ya awali mpaka ya mwisho ya ujenzi, pia aina zote za udongo zinaweza kutumika kwa utengenezaji wa matofali yanayofungamana ya udongo saruji, ila udongo ulio bora na mzuri kutumia ni ule wenye kiasi cha mfinyanzi kati ya asilimia kumi(10%) hadi asilimia arobaini(40%).

Aidha aliongeza kuwa ujenzi wa kutumia matofali haya hauhitaji matumizi ya Saruji ili kuyaunganisha bali hupangwa kwa mpangilio maalum unaowezesha kuta za jengo kushikamana kwa uimara kutokana na matundu yaliyomo kwenye matofali hayo.

Mpaka sasa Teknolojia ya matofali hayo imetumika katika ujenzi wa Majengo Mbalimbali kwenye Mikoa ya Morogoro, Iringa, Manyara, Tabora na Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment