TANGAZO


Tuesday, April 29, 2014

Wananchi waaswa kuzingatia usafi wa mazingira


Ofisa Mazingira wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke Bw.Ernest Mamuya akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani)kuhusu hatua zinazochukuliwa na Manispaa hiyo katika kuhakikisha  kuwa kanuni na taratibu za usafi wa mazingira zinazingatiwa na wananchi wote kwa kuyaweka mazingira yao katika hali  ya usafi ili kujikinga na magonjwa ya milipuko.


Ofisa Afya wa Manispaa ya Temeke Bw.Willium Muhemu akifafanua kwa waandishi wa habari mafanikio yaliyofikiwa na Manispaa hiyo katika kuwaondoa wafanyabiashara wanaofanya biashara katika maeneo yasiyo rasmi pamoja na watu wote wanaochafua mazingira,Kulia ni Afisa Uhusiano wa Manispa hiyo Bi. Joyce Nsumba. (Picha zote na Frank Mvungi-Maelezo)




Na Hassan Silayo-MAELEZO
Wananchi wameaswa kuzingatia usafi wa mazingira kwa kuwa jukumu la kila mwananchi kulinda na kutunza na kuzingatia kanuni za usafi wa mazingira.
Hayo yamesemwa na Afisa Afya wa Manispaa ya Temeke Bw. Willium Muhemu wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.
Bw. Muhemu alisema manispaa hiyo imeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha kuwa kanuni za usafi, taratibu na sheria za usafi wa mazingira zinazingatiwa na wadau wote wa mazingira ili kuepusha mlipuko wa magonjwa.
“Moja ya mikakati iliyowekwa na manispaa ya Temeke ni kuhakikisha kwamba hakuna mtu anayefanya biashara katika maeneo yasiyo rasmi ili kuzuia uchafuzi wa mazingira na yeyote atakaye kiuka utaratibu huo atachukuliwa uchafuzi wa mazingira” Alisema  Bw. Muhemu
Naye Afisa Mazingira wa Manispaa hiyo Bw. Ernest Mamuya alisema kuwa ili kuhakikisha kuwa manispaa hiyo inakuwa katika hali ya usafi wakati wote wanao mpango mpango wa kuongeza magari ya kubeba taka , kuwa na dampo la kudumu la kuhifadhia taka na kuhakikisha taka zinazolewa kwa wakati.
Akitoa wito kwa wananchi Bw. Mamuya alisema kuwa wananchi wanapaswa kuzingatia kanuni za usafi katika ngazi za familia ili kuunga mkono mpango wa manispaa katika utunzani wa mazingira.
Maafisa afya wa kata wanaendesha zoezi la ukaguzi wa nyumba kwa nyumba kwa kushirikiana na wajumbe wa kamati za afya za mitaa husika ili kuhakikisha kuwa wananchi wanazingatia kanuni za usafi.

No comments:

Post a Comment