Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba kutoka Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Moses Machari akizungumza na waandishi wa habari, mjini Dodoma leo, kuhusu alichodai kupotoshwa kwa masula kaadhaa juu yao na wale aliowataja wajumbe wa kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), ikiwemo kuzuliwa kuwatukana waasisi wa Muungano, Mwalimu Julius Nyerere na Abeid Amani Karume. (Picha zote na Kassim Mbarouk- www.bayana.blogspot.com)
Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba kutoka Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Moses Machari akizungumza na waandishi wa habari, mjini Dodoma leo, kuhusu alichodai kupotoshwa kwa masula kaadhaa juu yao na wale aliowataja wajumbe wa kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM), ikiwemo kuzuliwa kuwatukana waasisi wa Muungano, Mwalimu Julius Nyerere na Abeid Amani Karume.
Ndugu waandishi wa habari,
Leo tarehe 24/04/2014
nalazimika kukutana nanyi kwa lengo la kutoa ufafanuzi juu mambo mbalimbali ya
kizushi yanayotolewa ndani na nje ya ukumbi wa Bunge Maalum. Kwa ujumla
nitazungumzia mambo yafuatayo:
1.
Tuhuma ya kuchukua Posho na kuondoka
2.
Tuhuma ya Matusi na Ukosoaji wa Viongozi
mbalimbali.
3.
UKAWA kutumika na Mataifa ya Nje
4.
Kauli za Vitisho na Uchochezi unaofanywa na
wajumbe wa CCM (Kauli za Ndg. Damian Komba na William Lukuvi).
Ndugu Wanahabari,
Ni ukweli usiopingika
kwamba kumekuwepo na upotoshaji mkubwa sana ndani na nje ya bunge juu ya
wajumbe tulioamua kuahirisha kuendelea na vikao vya Bunge maalumu la katiba (Wana
UKAWA) baada ya kutoridhishwa na mwnenendo mzima wa vikao vya Bunge hilo. Kwa kuwa
sisi wajumbe tuliopewa jukumu la kuhakikisha tunaipatia nchi yetu katiba mpya
inayozingatia maslahi mapana ya nchi yetu; na kwa kuwa pamekuwepo na mionendo
ya kizushi iliyosheheni propaganda tele miongoni mwa Wajumbe wanaotokana na CCM
pamoja na wajumbe wengine ambao kimsingi ni
mawakala CCM; katika hali hiyo
kwa mtu yeyote mwenye akili nzuri na timamu asingeweza kuendelea kujenga hoja
yoyote katika mazingira ya fujo kama yale.
Ndugu Wanahabari,
Baadhi ya mambo mabaya
ambayo yametendeka katika Bunge Maalum kabla na hata baada ya wajumbe wa UKAWA
kuondoka ni pamoja na haya yafuatayo:
Kwanza, ni upotoshaji wa makusudi unaofanywa na CCM dhidi
UKAWA kwamba wajumbe wa UKAWA tumerudi bungeni kuchukua posho.
Ndugu wanahabari,
Jambo hilo si kweli na
ninapenda kuwahakikishia Watanzania kwamba hakuna mwana UKAWA hai aliyerejea
katika ofisi za bunge kudai posho wala kuchukua posho. Kauli ya upotoshaji kama
hiyo ni dalili za CCM na vibaraka wao kukosa hoja za kujibu hoja nzito za UKAWA zilizowasilishwa ndani ya Bunge maalumu
zilizohusu Muungano wetu. Itakumbukwa kwamba
mara tu baada ya UKAWA kutoka baadhi ya Ma-CCM walisema kwamba UKAWA wamechukua
posho za hadi tarehe 30 Aprili na kukimbia, lakini pia ikasemwa tena ndani ya
bunge kuwa UKAWA warudishe fedha za Wananchi walizochukua kwa siku ambazo
hawako bungeni, sasa unajiuliza nani hapa mkweli mara wamechukua, mara wanakuja
kuchukua, hii ni dalili ya kushindwa kuwa na hoja na kuamua kuchafua wajumbe wa
UKAWA, ilihali tulichokikataa ni kuwa na mjadala usioendana na rasimu ya katiba
iliyotokana na maoni ya wananchi. Maajabu ya maajabu ma-CCM wamekalia mipasho
na kutaka UKAWA tukae na watu waliopoteza mwelekeo katika mchakato huu wa
kuapata katiba mpya. Jambo hilo haliwezekani hadi watakapojisahihisha na
kuheshimu maoni ya wananchi yaliyowasilishwa na Tume ya mabadiliko ya katiba.
UKAWA ni watu makini na tusiokurupuka.
Lakini pili ndugu waandishi
wa habari, zimekuwepo tuhuma juu ya UKAWA kutumika na mataifa ya nje.
Ndugu zangu Wanahabri, kusimamia maoni ya
wananchi ni jukumu la kila kiongozi wa taifa lolote. Hivyo UKAWA hatutaweza
kushawishiwa kamwe na taifa lolote na hatutaweza kukoma kutetea maoni ya watanzania
kwani ndio msingi wa utawala wa kidemokrasia na maoni yaliyowasilishwa na Tume
ya Mabadiliko ya katiba kupitia mwenyekiti wake Jaji Joseph Sinde Warioba. Inaeleweka
bayana kuwa ma-CCM na wale vibaraka wao
wanataka kuwafanya UKAWA washindwe kusimamia maoni ya wananchi na badala yake
UKAWA tuendelee kujadili mambo mengine. Katika lugha nyingine, wajumbe wa CCM
wamedhamiria kuhamisha ajenda
iliyowafanya kuonekana hawana hoja za kupangua hoja za walio wachache ambao
wengi wao ni wafuasi wa UKAWA. Aidha tuhuma hizi nzito zilizotolewa na Ndg.
PAUL MAKONDA, tunazipuuza kwa kuwa tunaelewa wazi anatafuta umaarufu kwa
kupitia kuikashifu UKAWA. Hata hivyo Ndg. PAUL MAKONDA a.k.a mtafuta umaarufu
tunampuuza kwa kuwa tunamchukulia kama KIFARANGA cha kuku labda siku moja
akijitokeza mama au baba wa kifaranga tutamjibu na kumtaka athibitishe pasipo
kuacha shaka kwa kueleza ni nchi gani na namna gani UKAWA inatumika na mataifa
ya nje kutaka kuvuruga amani ya nchi yetu. Ninachoweza kusema katika hatua hii,
kama kuna Mwana CCM yeyote anayeweza kuthibitisha madai yaliyotolewa na Paul
Makonda ajitokeze na kuthibitisha tuhuma hizo pasipo kuacha shaka. UKAWA tuko
imara na hatuwezi kuyumbishwa na tuhuma za kipuuzi zisizokuwa na ukweli, tuna
akili nzuri na tunajua umuhimu wa nchi kuwa na amani na kamwe hatuwezi kukubali
vitendo vya uvunjifu wa amani hapa nchini. Lakini pia sidhani na sitegemei
kuona wajumbe wenzangu wa UKAWA wakikaa kimya kwa kuvumila upotoshaji wa aina
hii ukifanywa, bali ninashawishika kusema kwamba UKAWA itatumia umakini wake
kuhakikisha hatua sahihi zinachukuliwa dhidi ya mtu au kikundi chochote
kitakachofanya mambo yasiyokuwa na tija kwa maslahi mapana ya nchi yetu.
Ndugu wanahabari,
kumekuwepo na Tuhuma ya kwamba wana Ukawa wanatukana au wanatumia Matusi dhidi
ya waasisi wa muungano wetu. Napenda kueleza kwamba, UKAWA ni watu makini na
kamwe hatuwezi kuwatukana waasisi wa Muungano wetu lakini mimi kama mwana UKAWA
naweza kumkosoa mtu yeyote Yule wakiwemo waasisi wa muungano wetu kwa yale waliyoyafanya
na sitakiwi kutafsiriwa kuwa nimetukana kwa kuwa ipo tofauti kubwa sana ya
kukosoa na kutukana viongozi au mtu mwingine yeyote Yule. Kwa kuwa ma-CCM ni
wapenzi wa propaganda yaani upotoshaji; kamwe sitegemei kuona hata siku moja
katika uhai wangu wakikubali Ukweli wa mtu yeyote asiyekuwa mwana CCM kirahisi
kabla ya kutokea madhara makubwa. Ninyi na mimi ni mashahidi na tuna recods mbalimbali kuhusu Wabunge na
viongozi wa CCM kuukataa ukweli hadi madhara makubwa yajitokeze juu ya jambo
Fulani, kwa mfano masula ya OPERESHENI TOKOMEZA nk, walielezwa mapema lakini
hawakusikia hadi madhara makubwa yalipoonekana na kupigiwa kelele kwa kiasi kikubwa
ndipo wakachukua hatua kwa shinikizo kubwa ilihali watu walishapoteza maisha.
Kwa hiyo, kumkosoa mtu yeyote siyo matusi bali ni utamaduni wa kawaida kwa
jamii yoyote iliyostaarabika duniani. Hii ni kwa sababu haiwezekani binadamu akaishi
na kufanya maamuzi pasipo kukosea na kwa mantiki hiyo ni sharti akosolewe kwa
lengo la kujenga na siyo kubomoa.
Hivyo basi kumkosoa hayati
Mwl. NYERERE na Rais KARUME haikuwa kosa na wala hawa wazee wetu hawakuwa malaika
wala Miungu (Mungu) kiasi kwamba hakuna mahala walipotenda makosa; hilo
haliwezekani. Hivyo basi ni vema, CCM waache uvivu wa kufikiri na hivyo
kushindwa kutofautisha Matusi na kuwakosoa Waasisi wa Muungano wetu au viongozi
wengine walio hai hivi sasa. Mimi binafsi sijasikia na wala sijaona ni wapi
Wajumbe wa UKAWA waliwatukana wazee hawa bali walichokifanya baadhi ya wajumbe
wa UKAWA ni kukosoa makosa au dosari za muungano zilizosababishwa na hayati
Rais Nyerere na Karume ili katika mchakato huu wa Katiba Mpya tuweze kuziepuka
kasoro hizo na kuwa na MUUNGANO IMARA ZAIDI.
Hao wanaoendelea kusema
kwamba Mhe. TUNDU LISSU na wengine waliwatukana wazee hao ni mwendelezo wa
upotoshaji wanaoufanya kwa makusudi baada ya kuishiwa hoja za kutetea msimamo
wao wa serikali mbili. TUNDU LISSU na baadhi ya
wana UKAWA hawakutukana bali walikosoa
dosari au mapungufu ya muungano wetu katika kuanzishwa kwake. CCM na washirika
wao wa Propaganda wamwogope Mungu na watubu dhambi ya kusema uwongo ili
wasihukumiwe. Mbaya zaidi hata viongozi wa dini Mathalani Askofu Mkuu Mstaafu wa
Kanisa la Anglican Tanzania DONALD MTETEMELA na Shehe JONGO nao wameingia
katika orodha ya watu wanaosema uwongo hadharani pasipo kumwogopa Mungu.
Ninasema kwamba Tundu Lissu hajawatukana waasisi wetu bali aliwakosoa na akashauri
tuangalie dosari za muungano wetu ziko wapi na tuujenge upya ili kuondoa kero
za Muungano kwa pande zote mbili.
KAULI
ZA UCHOCHEZI MIONGONI MWA WANA CCM:
Ndugu wanahabari, ninyi na
mimi ni mashahidi kwamba pamekuwepo na Kauli
za Vitisho na Uchochezi unaofanywa na wajumbe wa CCM.Kwa mfano vitendo
vilivyofanywa na Waheshimiwa Wabunge/ Wajumbe WILLIUM V. LUKUVI na Kept.
DAMIANO KOMBA vya kutoa kauli za kutufarakanisha wananchi tulio na mapenzi mema
na nchi yetu inadhihirisha ni wazi watu hawa na chama chao CCM hawataki amani
na utulivu kidogo tulio nao vikaendelea kuwepo. Hii ni kwa sababu kauli zao
zinachochea hasira miongoni mwa watu na hatima yake ni kwamba watu wanaweza
kuamua kufanya lolote kutokana na uchochezi huo. Na Binafsi ninashangaa sana
kwa nini Serikali haijawachukulia hatua hadi sasa. Uongozi wa nchi yetu umekaa
kimya kana kwamba kauli walizozitoa ni nzuri kwa nchi yetu, wakati ni kauli
mbaya kwa mustakabali wa maisha ya sasa na ya baadaye. Kwa Mfano Mhe. LUKUVI
katika hotuba yake wakati wa kumsimika Askofu wa kanisa la Methodist Dodoma
alisema maneno yafuatyo:
“…tuwaache
Wanzanzibari wajitawale wenyewe na Tanganyika; Wanzanzibari kule walipo 95% ni
Waislamu. Tunataka wajitangazie serikali ya kiislamu kule, Mnajua madhara yake?
Wale waarabu watarudi; Watazalisha siasa kali kule watakuja kutusumbua. Mimi
najua, kabisa. Kwa hiyo ndugu zanguni mnaposikia mjadala kule kuna watu
wanajifanya kuwasemea kumbe wana nia nyingine. Zanzibar ni kisiwa na visiwa
vinasumbua…”.
Katika DVD yenye kauli hiyo,
Mhe. LUKUVI anadhihirisha wazi kana kwamba Waarabu
si watu au binadamu wema pamoja na Dini ya kiislamu hapa nchini jambo
ambalo siyo jema katika kujenga taifa linaloheshimu misingi ya umoja miongoni
mwa watu wenye imani tofauti za kidini. Nimejiuliza na bado ninajiuliza maswali
mengi: Je, kauli ya Lukuvi ni serikali nzima au ni yake binafsi? Nauliz hivi kwa kuwa siku hiyo alienda katika kanisa hilo kama mwakilishi wa Mhe. Waziri Mkuu ambaye
ndiye Kiongozi Mkuu wa Shughuli za Serikali. Swali la pili la kujiuliza, kwa
kuwa kauli ya Mhe. Lukuvi inaonesha kuwa na chembechembe za kuichukia dini ya
kiislamu na waarabu hapa nchini, Je, ni lini Tanzania ikawa nchi ya dini
nyingine zilizosalia kama Ukristo; Ubudha; Uhindu nk hadi aoneshe chuki ya wazi
dhidi ya Uislamu halafu serikali chini ya Mhe. Rais bado wanamuacha Mhe.
Lukuvi? Binafsi ninavyoelewa, ni kwamba nchi yetu na serikali yetu huendeshwa
kwa misingi ya kutofungamana na dini yoyote ile bali inatambua na kuheshimu
uwepo wa dini mbalimbali na imani za watu wa dini hizo. Mbali na hali hiyo,
Tanzania imekuwa ikishirikiana na mataifa mbalimbali duniani ikiwemo mataifa ya
waarabu na ya Kiislamu kwa Mfano ABUDHABI; OMANI; ILANI;KUWAIT; LIBYA nk. Nchi hizo zimekuwa na mchango mkubwa kwa nchi
yetu kwani zimekuwa zikitupatia misaada ya kifedha pasipo kujali Tanzania inayo
madhehebu mengine ya kidini kama vile Ukristo nk ambapo watu wa madhehebu yote
wamenufaika na misaada hiyo ya waarabu na waislamu wa nchi zimezowahi
kutusaidia. Ni Vema tukajiuliza Mhe. LULUVI anapata wapi uhalali na jeuri ya
kutoa kauli inayoonekana kuwa na mlengo wa kutoipenda dini ya kiIslamu na watu
wa jamii ya kiarabu wakati yeye ni kiongozi na maadili ya uongozi yanakataza
ubaguzi wa aina yoyote ile katika utekelezaji wa majukumu ya kila siku?
Mwisho kabisa, mimi na wana
UKAWA tumesikitishwa na kauli ya Kepteni Damiano Komba(Mb) ya kwamba ataingia
Msituni iwapo serikali mbili hazitaendelea kuwepo hapa nchini. Kauli hiyo ni
mwendelezo ule ule wa wa vitisho na kuwafanya Watanzania waishi kwa hofu lakini
pia kuwatia hasira wananchi Wenye mawazo tofauti na ule wa CCM wa kuendelea
kuwa na mfumo wa Muungano wa serikali mbili. Ni imani yangu kwamba kutishia
kwenda Msituni ni kauli mbaya na ya kichochezi kwa kuwa Matendo ya watu
walioamua kwenda msituni siyo mazuri hata kidogo. Tujifunze kwa wenzetu wa nchi
za DRC; BURUNDI; RWANDA;UGANDA; SUDANI KUSINI nk. Maisha yao yamekuwa ya hofu
mno katika nchi hizo.
Ndugu Wanahabri,
Kepteni Komba anataka kutuingiza
katika machafuko kwa sababu ya madai ya serikali tatu zilizopendekezwa na
wananchi kupitia Tume ya mabadiliko la katiba? Katika, hili ninatamka bayana
kwamba Mhe. Komba anapaswa kuchukuliwa hatua za kinidhamu kwanza na chama chake
lakini pia na serikali inayotuongoza ili kuepusha nchi isiingie kwenye machafuko.
Kauli za namna hiyo zinachochea hasira miongoni mwa watu. Uzalendo siyo kutoa
kauli za namna hiyo bali kutoa kauli zenye kuleta matumaini. Kwa kuwa chama
chake CCM kimefumba macho kwa kutokemea kauli hizo ni wazi siyo makosa kwa mtu
kutafsiri kwamba kauli za Akina Lukuvi na Kept. Komba ndiyo msimamo wa CCM na
kwa mantiki hiyo, inatubidi watanzania tusiyo wana CCM tutafakari hatua sahihi za kuchkua dhidi ya mtu
yeyote yule mwenye kutetea maslahi
mapana ya nchi yetu. Ni wazi CCM wanataka kuiingiza nchi yetu kwenye machafuko
kupitia kauli zinazotolewa na viongozi hao. Je, na sisi UKAWA tuseme kwamba
tutaingia msituni? P
Ndugu waandishi wa Watanzania
wote, sisi UKAWA ni watu tunaoheshimu utaratibu uliowekwa na katiba, sheria na
kanuni mbalimbali za nchi yetu. Tunawataka CCM kueleza ni kwa nini watu wake
wanatoa kauli za uchochezi hadharani? Ninawaeleza kwamba wasidhani kwamba UKAWA
tunatishika na kauli za namna hiyo, tuko imara na tutaendelea kudai katiba mpya
kwa hoja na ikitokea vinginevyo tutakabiliana na chama au mtu yeyote Yule kwa
namna yoyote na kwa gharama yoyote ili kuhakikisha hakuna dhulma na unyanyasaji
wowote. Tunawataka CCM na watu wake kuheshimu utaratibu unaotumika katika
kuendesha nchi yetu, na daima waelewe kwamba UKAWA siyo wajinga.
Ndugu, wanahabari, kupitia kwenu nina amini
kwamba ujumbe huu utawafikia wana CCM na hivyo kuwa chachu ya kuwafanya
watafakari upya kauli zao. Niwatoe hofu wananchi wote kwa kusema kwamba UKAWA
hatutarajii kuona uvunjaji wa taratibu za nchi yetu bali tunatarjia kuona kila
mtu au kikundi chochote kile kikiheshimu sheria zilizopo ili kuiepusha nchi
yetu kuingia kwenye matatizo. Ni aibu watu wazima wamekalia propaganda badala
ya kujadili rasimu kama dhamira yao ni njema. UKAWA hatukutoka nje kwa kupenda,
na wala baada ya kutoka hatukwenda “picnic” bali tulitoka kwa sababu ya tabia
chafu ya Wajumbe wa CCM na mawakala wao ya kutoa kauli za mipasho na kejeli badala ya kujadili
Rasimu ya Katiba iliyokuwa mezani. Waingereza wanasema “ Don’t argue with a
fool because others may not see the difference” Katika mazingira kama yale
UKAWA tungeendelea kubishana na watu wenye shingo ngumu kama wale wote
tungeonekana kuwa na matatizo ya kufikiri jambo ambalo sisi UKAWA hatukubali
kubeba ujinga wa wengine.
Hata baada ya sisi wana
UKAWA kuondoka kinachoendelea Bungeni hivi sasa, ni upotezaji wa muda na fedha
za walipa kodi masikini wa Tanzania.
Sisi wana UKAWA kwa kutambua umuhimu wa Katiba laikini pia kwa kutambua kuwa
wananchi wetu bado ni masikini hatukupenda kutumia fedha ya umma bure. Hivyo
tuliacha posho na tukaamua kwenda kwenda kwa wananchi kuwaeleza uozo
unaoendelea bungeni ili hatimaye tuweze kupata ushauri wa wananchi juu ya nini kifanyike. CCM wanatubeza, lakini
niseme tu katiba yoyote ile inatakiwa kupatikana kwa maridhiano.
Nawashkuru sana na asanteni
kwa kunisikiliza
……………………….
Moses Joseph Machali (mb)
MBUNGE
WA KASULU MJINI NA MJUMBE WA BUNGE MAALUM
24/04/2014
No comments:
Post a Comment