TANGAZO


Friday, November 8, 2013

Taasisi ya Chakula na Lishe yaelezea mpango wake wa uongezaji wa virutubisho kwenye vyakula, kusaidia kuondoa magonjwa yanayosababishwa na upungufu wa lishe

Ofisa Lishe Mwandamizi wa Taasisi ya Chakula na Lishe, Maria Msangi, akieleza kwa waandishi wa habari (hawapo pichani), kuhusu utekelezaji wa mpango wa uongezaji wa virutubisho kwenye vyakula ili kusaidia kuondoa magonjwa yanayosababishwa na upungufu wa lishe, wakati wa mkutano uliofanyika, ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Dar es Salaam leo. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Sayansi wa Taasisi hiyo, Dk. Elifatio Towo. (Picha na Hassan Silayo-MAELEZO)
 
Na Georgina Misama-MAELEZO
Taasisi ya Chaula na Lishe yaiasa jamii kuzingatia lishe bora kuanzia  kipindi cha ujauzito hadi mtoto anapofikisha miaka miwili.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Sayansi ya Chakula na Lishe (TFNC) Dkt Elifatio Towo wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam.

Dkt  Towo alisema kuwa uzingatiaji wa lishe bora utachangia katika kutokomeza utapiamlo na kuimarisha afya ya mtoto tangu akiwa tumboni kwa mama na kudumu kwa maisha yake yote.

“Watoto  waliopata lishe ya kutosha na hasa katika kipindicha siku 1000 za mwanzo tangu mama anapokuwa mjamzito mpaka mtoto anapofikisha miaka 2 wanakuwa wamepata faida zitakazodumu katika maisha yao yote” alisema  Dkt Towo.

Aidha aliongeza kuwa uongezaji wa Vitamini na Madini  kwenye vyakula ni muhimu katika utendaji kazi wa mwili kwa watoto walio chini ya umri wa miaka 5 na wanawake  walio katika umri wa kubeba mimba.

Alifafanua kuwa  tafiti zinaonesha  kuwa asilimia 59 ya watoto chini ya umri wa miaka 5, na asilimia 41 ya kina mama wana upungufu wa madini chuma yanayopelekea kushusha kiwango cha utengenezaji damu.

 Akieleza namna ya kukabiliana na tatizo hilo, Dkt Towo alisema kuwa, Taasisi imeanzisha  teknolojia ya uongezaji wa vitamin na madini katika vyakula vikuu kama vile unga wa ngano, sukarik mafuta ya kula, na unga wa mahindi.

Akijibu swali la mwandishi alietaka ujua licha ya kuwepo kwa vyakula mbalimbali kwanini baadhi ya watoto wanaandamwa na magojwa, Afisa Mwandamizi wa Sayansi ya Lishe Maria Msangi alisema kwamba lishe duni inasababisha kinga hafifu  na kupelekea jamii yenye kuandamwa na magonjwa hasa ya kuambukizwa.   

Uzinduzi wa Mpango kuongeza virutubishi  kwenye vyakula ulifanywa na Mheshimiwa Rais wa Jamuhuri ya Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na tayari vyakula hivyo vinapatikana kwenye maduka na sokoni vikiwa na nembo maalum inayoonyesha vyakula hivyo vimeongezwa virutubisho.

No comments:

Post a Comment