TANGAZO


Thursday, October 24, 2013

Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini yaelezea mikakati yake ya kuongeza idadi ya wananchi waliosajiliwa na kupata vyeti vya kuzaliwa nchini

Wakili wa Serikali toka Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), Patricia Mpuya akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani), kuhusu maboresho ya Sheria ya Usajili wa Vizazi na Vifo, itakayowezesha kusogeza huduma za upatikanaji vyeti vya kuzaliwa karibu na maeneo ya wananchi, pia kuongeza idadi ya wananchi waliosajiliwa, wakati wa mkutano uliofanyika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) leo, jijini Dar es Salaam.
Meneja Masoko na Mawasiliano wa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA), Josephat Kimaro akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani), kuhusu mikakati ya wakala hao ya  kuongeza idadi ya wananchi waliosajiliwa na kupata vyeti vya kuzaliwa nchini, wakati wa mkutano uliofanyika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) leo, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa Habari wa Idara ya Habari (MAELEZO), Georgina Misama. (Picha zote na Eliphace Marwa-MAELEZO)

UTANGULIZI
Cheti cha kuzaliwa ni moja ya nyaraka muhimu sana kwamaisha ya kila mwananchi kwani humsaidia kupata huduma mbalimbali za msingi. Kisheria hii ni nyaraka pekee inayotambulisha mtu, tarehe aliyozaliwa na hivyo umri wake.Pamoja na umuhimu wanyaraka hii, bado ni idadi ndogo ya asilimia 23 yaWatanzania wamesajiliwa na kupata vyeti vya kuzaliwa.

Idadi hii ndogo inatokana na sababu za kihistoria kwani huduma hii imeanza kutolewa kabla ya uhuru na wakati huo ilitolewa kwa wageni tu.Pia sheria ya usajili inayotumika si rafiki kiasi cha kuwawezesha wananchi wengi kupata cheti cha kuzaliwa.

MIKAKATI
Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA), Taasisi ya serikali iliyo na jukumu la kusimamia usajili wa Vizazi na vifo,umeendelea kutekeleza mikakati mbalimbali yenye lengo la kuhakikisha idadi ya wananchi waliona vyeti vya kuzaliwa inaongezeka kwa kusogeza huduma karibu zaidi na maeneo ya makazi ya wananchi.

Mikakati hiyo ni pamoja na

1)  Kuipitia na kuiboresha sheria ya Usajili wa vizazi na Vifo

Wakala umeanza mchakato wakuwezesha kupatikana kwa sheria mpya itakayochukua nafasi ya Sheria ya Vizazi na Vifo sura na 108 ya mwaka 1920 ambayo ilifanyiwa marekebisho ya mwisho mwaka 2009 inayotumika kwasasa.

Sheria mpya inakusudia kusogeza huduma za upatikanaji vyeti vya kuzaliwa karibu na maeneo ya wananchi, matumizi ya teknolojia katika kutuma na kutunza taarifa za usajili, kufanya mapitio ya ada za vyeti vya kuzaliwa, kuongeza adhabu kwa wanao thibitika kuwa na vyeti bandia vya kuzaliwa, nk. Rasimuya kwanza ya Sheria mpya imeshatoka na kupiti wa na wadau.

2) MkakatiwaUsajiliwaWatotowalionaUmriChiniyaMiakaMitano( U5BRI).

Mkakati huu unatekelezwa kwa awamu na tayari umeanza kutekelezwa katika Mkoa wa Mbeya kuanzia mwezi Julai 2013 na kuonyesha mafanikio makubwa.U5BRI unategemea kuendelea kuenezwa katika mikoa yote ya Tanzania Bara.

Nguzo za mkakati huu ni pamoja na

·        Kusajili na kutoa vyeti kwa watoto chini ya Miaka Mitano katika Ofisi za Watendaji kata na vituo vya tiba.

·        Kuondoa ada ya cheti kwa kundi hilo

·        Kutumia teknolojia ya mawasiliano katika kutuma na kutunza taarifa

3) KupunguzamudawaupatikanajiwaVyetivyakuzaliwa

Miaka ya Nyuma ilimchukua mwananchi si chini ya mwezi mmoja kuanzia kuomba mpaka kupata cheti cha kuzaliwa.Kwasasa baadhi ya mifumo imeboreshwa hivyo mwananchi ataweza kuomba nakupata cheti ndani ya wiki moja.Maboresho zaidi yanaendelea kufanyika ili kupunguza zaidi idadi ya siku. 

4)  MkakatiwaUsajilinakutoavyetivyakuzaliwakwaWatotoMashuleni

Mipango inaendelea kuanza usajili kwa wanafunzi wote wa shule za Msingi mkoani Dar es Salaam. Kwa kuanzia zoezi hili litafanyika katika Wilaya ya Ilala kwa kushirikiana na Idara ya Elimu ya Wilaya.

5)     KampenizaUsajilinakutoaVyetivyaKuzaliwakatikaWilaya

Kampeni hizi zimekuwa zikifanyika kwa muda mrefu na zinaendelea kufanyika katika wilaya mbalimbali. Kwa mwaka huu,kampeni zimeshafanyika katika Wilaya 15 za mikoa mbalimbali

6)     UsajilinakutoaVyetivyaKuzaliwakatikaTaasisi

Wakala umeanza kutoa huduma ya usajili katika makundi maalumu ambapo hujaza fomu za maombi nakupatiwa vyeti vya kuzaliwa katika maeneo waliko baada ya kupitia hatua zote stahili.

Mpaka sasa huduma hii imeshatolewa katika taasisi 42 za Mkoa wa Dar es Salaam nyingi zikiwaTaasisi za Majeshi ya Ulinzi na Usalama, taasisi za kidini, Wizara, Makampuni na mashirika mbalimbali.

7)     ElimukwaUmma

Wakala unaendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa Usajili, wapi huduma zinapatikana, vigezo husika Nk. Programu mbalimbali za elimu kwa umma zinaandaliwa ili wananchi wajue faida ya kuwa na cheti cha kuzaliwa


HITIMISHO
Sheria mpya inategemewa kutamka ulazima wa kila mwananchi kuwa na cheti cha kuzaliwa na kusisitiza matumizi yake katika sehemu zote zinazohitaji uthibitisho wa umri. Kila mwananchi aliyezaliwa katika ardhi ya Tanzania Bara anayo haki yakusajiliwa nakupata cheti kwa mujibu wa Sheria.

 RITA inawaomba wananchi wote waliozaliwa Tanzania Bara kujisajili ilikupata vyeti vya kuzaliwa na vinapatikana bila usumbufu na kwa muda mfupi. Wananchi wanatakiwa kufika wenyewe katika ofisi za Wakala nawaepuke kutumia vishoka au madalali“vishoka”wanaotoa vyeti visivyotambulika‘’feki”hivyo kusababisha Usumbufu.Pia Wakala unazikumbusha taasisi mbalimbali zinazotumia Cheti cha Kuzaliwa kama moja ya kiambatanisho kuvileta kwa ajili ya kuvihakikii likuweza kubaini vyeti vya kughushi
Asanteni sana,
Imetolewana:
IDARA YA MASOKO NA MAWASILIANO
WAKALA WA USAJILI UFILISI NA UDHAMINI (RITA)

No comments:

Post a Comment