TANGAZO


Saturday, August 31, 2013

Mandela hakutolewa hospitali


Picha ya Mandela ikipambana ukuta Johannesburg siku yake ya kuzaliwa, 18th July
Serikali ya afrika Kusini imekanusha taarifa za vyombo vya habari kwamba aliyekuwa kiongozi wa afrika Kusini, Nelson Mandela, ambaye amelazwa hospitali tangu mwezi wa Juni, kwamba alirejeshwa nyumbani Johannesburg Ijumaa usiku.
Taarifa ya serikali imesema kuwa Bwana Mandela bado yuko hospitali mjini Pretoria na kwamba bado mahtuti, lakini hali yake imetulia.
Kulazwa kwa muda mrefu kwa kiongozi huyo kumewatia wasiwasi raia wa taifa hilo na ulimwengu kwa jumla.
Mandela ambaye ana umri wa miaka 95, alikuwa Muafrika wa kwanza kuwa rais wa taifa la Afrika Kusini, na anaheshimiwa na wengi kama baba wa taifa.

No comments:

Post a Comment