TANGAZO


Saturday, April 20, 2013

Azam FC, AS FAR Rabat zashindwa kufungana mchezo wa kwanza raundi ya pili Kombe la Shirikisho barani Afrika jijini Dar es Salaam

Mashabiki wa Azam FC, wakifuatilia na wengine kuishangilia timu yao, wakati timu yao hiyo, ilipopambana na AS FAR Rabat ya Moroco, katika mchezo wa kwanza wa raundi ya pili ya michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam leo. (Picha zote na Kassim Mbarouk)


David Mwantika wa Azam FC, akiudhibiti mpira huku akifuatwa na Salaheddine Said wa timu ya AS FAR Rabat ya Moroco, wakati wa mchezo wa kwanza wa raundi ya pili ya michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam leo. Hata hivyo timu hizo zimeshindwa kufungana katika mchezo huo.


David Mwantika wa Azam FC, akiudhibiti mpira huku akizongwa na Salaheddine Said wa timu ya  AS FAR Rabat ya Moroco, wakati wa mchezo wa kwanza wa raundi ya pili ya michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam leo. 


Humphrey Mieno wa Azam FC, akiufuata mpira uliokuwa ukiwaniwa pia na mchezaji Younes Bellakhadar wa AS FAR Rabat ya Marocco.

Khamis Mcha wa Azam FC, akijaribu kumpiga chenga Salaheddine Said wa timu ya  AS FAR Rabat ya Moroco.

Khamis Mcha wa Azam FC, akiwatoka Salaheddine Said na Younes Bellakhadar wote wa timu ya  AS FAR Rabat ya Moroco katika mchezo huo.

Salum Aboubakar wa Azam FC, akiwatoka wacheaji timu ya  AS FAR Rabat ya Moroco katika mchezo huo.

Mashabiki waliojaribu kuingia kwenye mchezo huo kwa njia zisizo halali wakiwa wamefungwa mashati kuongozwa na askari kanzu kupelekwa kituo cha Polisi Chang'ombe jijini Dar es Salaam.

Abderrahim Achichakir wa AS FAR Rabat, akiutuliza mpira huku nyuma akifuatwa na Humphrey Mieno wa Azam FC, wakati wa mchezo huo.

Younes Hammal wa AS FAR Rabat ya Morocco, akijaribu kumpiga chenga John Bocco wa Azam FC ya Tanzania atika mchezo huo.

Mcha Khamis wa Azam FC, akimtoka Younes Bellakhadar wa AS FAR Rabat ya Morocco katika mchezo huo.

Heka heka langoni kwa timu ya AS FAR Rabat ya Moroco, golkipa wa timu hiyo, Ali Grouni (kushoto), akiruka juu kuuondoa mpira wa hatari ulioelekezwa langoni kwake huku Younes Hammal (4), akiruka juu kujaribu kuondoa hatari hiyo.

Wazimri Salum wa Azam FC ya Tanzania, akiwatoka Younes Bellakhadar na Mohammed El Bakkali, wote wa AS FAR Rabat ya Morocco katika mchezo huo.

Kipre Tchetche wa Azam FC, akijaribu kumpiga chenga Hicham El Fathi wa AS FAR Rabat ya Morocco.

Waziri Salum akimtoka Hicham El Fathi wa AS FAR Rabat ya Morocco katika mchezo huo, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam leo.

No comments:

Post a Comment