Waandishi wa habari wakipokea taarifa hiyo.
|
Mwakilishi kutoka Kituo cha Usuluhishi (CRC), Elizabeth Muhangwa, akisisitiza jambo kwa waandishi wa habari.
|
Viongozi wa Mashirika ya kutetea haki za binadamu wakipitia ripoti hiyo. (Picha zote na Habari namwaibale.blogspot)
Na Dotto Mwaibale
Utafiti uliofanywa na mashirika ya kutetea haki za binadamu
katika utafiti wa awali kuptia mradi wa Gewe II kuhusu
ukatili wa kijinsia hapa nchini umebaini waathirika wa
matukio hayo hawana sehemu maalum ya kupeleka
malalamiko yao.
Hayo yamesemwa Dar es Salaam leo Mkurugenzi
Mtendaji wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake
Tanzania (TAMWA),
Valeria Msoka, wakati akizungumza na waandishi wa
habari wakati akitoa taarifa ya utafiti wa awali za
ukatili wa kijinsia.
Alisema utafiti huo umefanywa na Mashirika matano
ya kutetea haki za Binadamu ambayo ni Chama cha
Wanasheria wanawake (TAWLA), Chama cha
Wanasheria wanawake Zanzibar (ZAFELA),
Kituo cha Usuluhishi (CRC), Mtandao wa Jinsia
Tanzania (TGNP) na Chama cha waandishi
Habari wanawake Tanzania (TAMWA)
Bara na Zanzibar.
Alisema utafiti huo umeonesha asiliamia 17 ya wananchi wanauelewa wa sheria za ukatili hali imayopelekea
kutokufuatilia haki zao wakati wa uvunjaji na
wakati mwingine kutoripoti kabisa kesi hizo.
Alizitaja wilaya zilizofanyiwa utafiti ghuo kuwa ni
Wete (Pemba kaskazini), Magharibi Unguja, Kusini
Unguja (Kusini Unguja), Kisarawe (Pwani),
Newala (Mtwara), Lindi Vijijini (Lindi), Mvimero
(Morogoro) na wilaya mbili za Kinondoni na Ilala
(Dar es Salaam).
Msoka aliitaja Lindi Vijijini kuwa ndio wilaya
inayoongoza
kuwa na uelewa mdogo wa asilimia 12 ambapo
asilimia 21 ya uelewa kwa Wete Zanzibar kuwa
ni mkubwa kuliko wilaya zote ulipofanyika utafiti huo.
"Ofisa mmoja wa Polisi Lindi alisema kesi nyingi
huripotiwa katika hatua ya familia na hufikishwa
mahakamani baada ya kushindwa kupata suluhu hivyo
kuwa katika hatari ya kupata haki" alisema Msoka.
Aliongeza kuwa utafiti huo kwa ujumla uliona
asilimia 47 za kesi huripotiwa katika Serikali za vijiji,
asilimia 25 huripotiwa polisi nyingine huripotiwa
Kamisheni ya Haki zaaa Binadamu, Mashirika
ya Hakli za Binadamu na kwa wanasheria
wanaongoza (Para Legals).
"Hali hiyo ya kutokuwa na mfumo maalum wa kuripoti
inaweka mazingira ya kutopatika kwa haki na pia
kukosekana kwa takwimu sahihi ya kesi za ukatili"
alisema Msoka.
Alisema taarifa hiyo inaonesha kuwa wananchi
hawana majukwa ya kukaa pamoja na kujadili
changamoto zao am,bapo ni asilimia 13.5 ndiyo
wanachama wa vyama vya kijamii
(Civil Society Associations).
Msoka alisema kwa pamoja Mashirika hayo yatekeleza mpango wa Usawa wa Jinsia na Uwezeshaji wa Wanawake (GEWE) ambao unafanywa kwa mashirikiano na Serikali ya Denmark.

No comments:
Post a Comment