TANGAZO


Sunday, January 27, 2013

Wafaransa waelekea Timbuktu

Wanajeshi wa Ufaransa wanasonga mbele kuelekea mji wa Timbuktu ulioko katika jangwa la kaskazini mwa Mali, moja kati ya miji michache iliyobaki mikononi mwa wapiganaji wa Kiislamu.
 
Wapiganaji nje ya  mji wa Timbuktu

Mwandishi wa BBC nchini Mali anasema Wafaransa wanatarajiwa kuikomboa Timbuktu bila ya tatizo.

Ndege za Ufaransa piya zimeshambulia mji wa Kidal ambako ndiko wapiganaji walianza uvamizi wao mwezi Machi mwaka jana.

Jumamosi wanajeshi wa Ufaransa na Mali waliukomboa mji wa Gao uliokuwa ngome ya wapiganaji.
Na Mali ndio swala muhimu linalojadiliwa kati ya viongozi wa nchi za Umoja wa Afrika, AU, wanaokutana mjini Addis Ababa, Ethiopia.

Sasa nchi zaidi za Afrika zinatarajiwa kuchangia wanajeshi katika kikosi cha kimataifa kitachokwenda Mali, mbali ya wale walioshafika nchini humo.

No comments:

Post a Comment