
Waasi wa M23
Mazungumzo ya kuleta amani kati ya kundi la M23 na serikali
mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yanarejelewa tena hii leo mjini
Kampala Uganda.
Kundi hilo la M23 limetishia kujiondoa kwenye mazungumzo hayo hadi pale rais Joseph Kabila atakaposaini mkataba wa kusitisha mapigano.
Msemaji wa serikali ya Congo ameliambia shirika la Habari la Reuters kuwa limepuuza masharti hayo ya waasi kwa kuwa hayana msingi wowote.
Mazungumzo ya kujaribu kutatua mzozo huo uliodumu kwa zaidi ya miezi tisa yaliyofanyika mwaka uliopita yalisambaratika, baada ya wawakilishi wa pande hizo mbili kushindwa kuafikiana.
Inakisiwa kuwa zaidi ya watu laki nane wamekimbia makwao tangu waasi hao kaunzisha vita dhidi ya serikali ya nchi hiyo mwezi Mei Mwaka uliopita, kwa tuhuma za kupuuza mkataba uliokuwa sainiwa awali wa kuwashirikisha katika jeshi la serikali.
Waasi wadai kutaka kuimarisha hali ya maisha

Jean-Marie Runiga
Waasi hao waliuteka mji wa Goma, mwezi Novemba lakini walijiondoa kufuatia shinikizo za kimataifa.
Kiongozi wa shughuli za kisiasa wa waasi hao, Jean-Marie Runiga, aliwaambia waandishi wa habari kuwa serikali ya Congo, haikuwa imetimiza mapendekezo yake ya kusitisha mapigano na kuwa wanajeshi wa serikali wamekuwa wakijiandaa kuwashambulia.
Kundi hilo la M23 limeshutumiwa na Umoja wa mataifa kwa kufanya maasi dhidi ya raia jambo ambalo kiongozi wake Jean Marie Runiga amekanusha.
M23 imesema iataka kuimarisha hali ya maisha ya watu wa Mashariki mwa Congo, lakini Umoja wa Mataifa umedai kuwa waasi hao wanaungwa mkono na serikali za Rwanda na Uganda, madai ambayo yamekanusha vikali za serikali hizo mbili.
No comments:
Post a Comment