TANGAZO


Tuesday, January 8, 2013

Vyama vya Siasa, vyaendelea kuwasilisha maoni yao kwa Tume ya Katiba


Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Ussi Khamis, akizungumza katika mkutano na Viongozi wa Chama cha Kijamii (CCK), uliofanyika katika Viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam, wakati viongozi wa Chama hicho, walipowasilisha maoni yao, kuhusu Katiba Mpya leo, Jumanne Januari 8, 2013.


Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba,  Esther Mkwizu, akizungumza katika mkutano na Viongozi wa Chama cha Kijamii (CCK), uliofanyika katika Viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam, wakati viongozi wa Chama hicho, walipowasilisha maoni yao, kuhusu Katiba Mpya leo, Jumanne, Januari 8, 2013.

Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Dk. Salim Ahmed Salim, akizungumza katika mkutano na Viongozi wa Chama cha Kijamii (CCK), uliofanyika katika Viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam, wakati viongozi wa Chama hicho, walipowasilisha maoni yao, kuhusu Katiba Mpya leo, Jumanne, Januari 8, 2013.

Mwenyekiti wa Chama cha Kijamii (CCK), Constantine Makitanda, akizungumza  katika mkutano uliofanyika katika Viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam na Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, mara baada ya viongozi wa  Chama hicho, walipowasilisha maoni yao, kuhusu Katiba Mpya leo, Jumanne, Januari 8, 2013.


Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Riziki Mngwali, akizungumza katika mkutano uliofanyika katika viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam, baina ya Tume hiyo na Chama cha Wakulima (AFP), wakati ujumbe wa Chama hicho, ulipowasilisha maoni yao, kuhusu Katiba Mpya leo, Jumanne, Januari 8, 2013.

Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Raza Hamad, akizungumza katika mkutano uliofanyika katika viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam, baina ya Tume hiyo na Chama cha Wakulima (AFP), wakati ujumbe wa Chama hicho, ulipowasilisha maoni yao, kuhusu Katiba Mpya leo, Jumanne, Januari 8, 2013.


Katibu Mkuu wa Chama cha Wakulima (AFP), Rashidi Mohamed akiwasilisha maoni yao, kuhusu Katiba kwa Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika mkutano uliofanyika katika Viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam leo, Jumanne, Januari 8 2013.

Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba (kulia), akizungumza na Viongozi wa Chama cha Union for Multiparty Democracy (UMD), waliofika katika Ofisi za Tume hiyo leo, Jumanne, Januari 8, 2013, kuwasilisha maoni yao, kuhusu Katiba Mpya. Wa pili kulia ni Katibu wa Tume, Assaa Rashid na kushoto ni Viongozi wa Chama hicho, Juma Shariff na Moshi Kigundu.

Baadhi ya Viongozi wa Chama cha Union for Multiparty Democracy (UMD), wakifuatilia mkutano baina yao na Tume ya Mabadiliko ya Katiba leo, Jumanne, Januari 8, 2013, ambapo Uongozi wa Chama hicho, uliwasilisha maoni ya Chama hicho, kuhusu Katiba Mpya.
Katibu wa Chama cha Union for Multiparty Democracy (UMD), Juma, akizungumza wakati wa mkutano, uliofanyika leo, Jumanne, Januari 8, 2013, baina ya Chama hicho na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ambapo Chama hicho, kiliwasilisha maoni yao, kuhusu Katiba Mpya. Kulia ni Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Joseph Warioba na Katibu wa Tume, Assaa Rashid.
(Picha zote na Tume ya Katiba)

No comments:

Post a Comment